DC AWAONYA VIONGOZI WA VIJIJI WATAKAO ONGEZA BEI YA MAZAO CHAKULA CHA WANAFUNZI.

 

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu akizungunza na wananchi Kijiji cha Mpembe Kata ya Katuma.

Na Walter Mguluchuma- Tanganyika

Mkuu wa  Wilaya ya Tanganyika  Onesmo  Buswelu amewaonnya viongozi   wa  Vijiji  kuacha tabia ya kuuza ardhi   bila  utaratibu kwani kufanya hivyo  ni kinyume na sheria na taratibu na hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa wote watakao bainikaikiwemo kuwafikisha Mahakamani.

Baadhi ya Wakazi wa Kijiji cha Mpembe Kata ya Katuma wakimkiliza Mkuu wa Wilaya ya Tangayika Onesmo Buswelu

Mkuu wa  Wilaya ya Tanganyika  Onesmo  Buswelu amewaonnya viongozi   wa  Vijiji  kuacha tabia ya kuuza ardhi   bila  utaratibu kwani kufanya hivyo  ni kinyume na sheria na taratibu na hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa wote watakao bainikaikiwemo kuwafikisha Mahakamani.

Maagizo hayo ameyatoa wakati alipokuwa akiwahutubia wananchi wa  Kijiji  cha  Mpembe  Kata  ya Katuma wakati wa  maadhimisho  ya Wiki ya    Maji  iliyofanyika  kiwilaya  kwenye  Kijiji  hicho mara baada ya kuwa amezindua  huduma ya maji  kwenye  Kijiji hicho na upandaji wa miti .

DC  Buswelu  amesema kumekuwa na tabia ya  badhi ya  viongozi wa  Serikali za   vijiji kuuza  maeneo ya  ardhi   na   bila kufuata  utaratibu  na wengine wamekuwa wakiwauzia watu  mpaka  maeneo ambayo  yamehifadhiwa  jambo  ambalo  limekuwa  likileta  uharibifu wa  mazingira .

Amesisitiza kuwa  kwa   viongozi  wenye tabia  hiyo wahakikishe wanaacha  mara moja kuuza   ardhi bila kufuata utaratibu  na watakao bainika kufanya  hivyo hata kuwa na  huruma nao hata kidog atawachukulia hatua kama na kuwafikisha  Mahakamani .

Amesema  swala  la utunzaji wa  mazingira  ni la kipaumbele  katika  Wilaya  hiyo na  ndio  maana kuna  vijiji     nane  kwenye  Wilaya  hiyo ninanufaika   na         fedha   za  hewa ya  ukaa  kikiwepo na  Kijiji  hicho cha  Mpembe  ambacho kinatarajia  hivi karibuni  kupata  zaidi ya  shilingi  Bilioni  moja za  fedha ya  ukaa.

Aidha  Buswelu  amewataka  viongozi wa  vijiji  na   kamati za  shule   za     Vijiji  vinane  ambavyo  wanafunzi wa  wananufaika  kupa  chakula  shuleni kutokana na  fedha  za hewa ya ukaa  kuacha  mara moja tabia ya  kununua  vyakula  kwa  bei za juu  kwani  anazo taarifa  kuna  viongozi wamepanga kununua   gunia  moja    la  mahindi kwa  bei ya tshs 100,000  wakati gunia moja kwa sasa  ni tshs 30,000 kwenye  baadhi ya  vijiji.

Hivyo  amewaagiza TAKUKURU  kuhakikisha wanafatilia  ununuzi wa    vyakula vya wanafunzi  kwenye  vijiji hivyo nane kufuata mwongozo na kutoongeza bei ili kuweza kuwabaini watao taka  kujinufaisha wao binafsi kwa kupitia  fedha hizo  kwani Serikali ya  Wilaya ya Tanganyika   haiko   tayari kuona wananchi  wanaolinda  misitu nakufanyiwa hujuma .

Buswelu amemuomba  Mungu   amsimamie  na  amwongoze  na  amlinde  ili  aweze  kuwadhibiti  viongozi watao  jaribu    kupandisha  bei    ya    vyakula  vya wanafunzi shuleni .

Nae  Mkazi wa  Kijiji  cha  Mpembe  Benjamini   Masanja  amesema   wanamshukuru Rais  Dkt   Samia  Suluhu  Hassan  kwa kuweza kuwaletea  huduma  mbalimbali  kijijini hapo  kama  vile     huduma ya  maji safi na salama  ambayo hapo awali walikuwa hawana .

 Hivyo kutokana  na umuhimu wa  uhifadhi wa  mazingira  wananchi wa  Kijiji  hicho  wataendelea  kulinda  mazingira  ili  yasiweze   kuharibika .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages