SERIKALI MPANDA INATAMBUA MCHANGO WA SEKTA YA MADINI

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph akiwahutubia wadau wa Sekta ya Madini Wilaya ya Mpanda kwenye kikao hicho.

Na Walter Mguluchuma-Mpanda

Serikali ya Wilaya ya Mpanda   katika Mkoa wa Katavi  imesema kuwa inatambua kazi kubwa inayofanywa na wadau   sekta ya  madini    hasa wachimbaji wadogo, wakati na wakubwa  katika kukuza uchumi wa Mkoa na wa Nchi kwa ujumla    na kwa mwananchi mmoja  mmoja.

Wadau wa Sekta ya Madini Wilaya ya Mpanda wakiwa kwenye kikao hicho cha wadau wa sekta ya Madini Wilaya ya Mpanda.

Serikali ya Wilaya ya Mpanda   katika Mkoa wa Katavi  imesema kuwa inatambua kazi kubwa inayofanywa na wadau   sekta ya  madini    hasa wachimbaji wadogo, wakati na wakubwa  katika kukuza uchumi wa Mkoa na wa Nchi kwa ujumla    na kwa mwananchi mmoja  mmoja.

Kauli hiyo imetolewa na  Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  Jamila Yusuph  wakati wa kikao cha Jukwaa la wadau wa madini  Wilaya ya Mpanda kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Mpanda social Hall .

Amesema wanawapongeza wachimbaji wote wadogo  ,wakati na wakubwa walioko  katika  Wilaya ya Mpanda  kwa kazi kubwa  wanayofanya ya kuinua  uchumi wa wananchi wa Mkoa wa Katavi  na kuwapatia ajira wananchi  walioko kwenye maeneo ya uchimbaji.

Haidary Sumry Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mpanda akielezea mchango wa sekta ya madini kwa ukuaji wa Manispaa ya Mpanda.

Amebainisha kuwa Jukwaa hilo la wadau wa madni linaumuhimu sana kwa ajiri ya ustawi wa  maendeleo ya wananchi  wa wilaya ya Mpanda na Mkoa wa Katavi katika ukuaji wa uchumi.

Amesema  kwa mwaka 2024/2025 ofisi ya madini katika Mkoa wa Katavi  walipangiwa kukusanya  kiasi cha shilingi  bilioni 7 lakini   hadi sasa wameisha vuka lengo kwa kukusanya  7.2 ambazo ni sawa na asilimia 103 mapato hayo ya madini mengi yametoka katika Wilaya ya Mpanda .

DC  Jamila amemshukru  Rais   Dkt Samia Suluhu  Hassan  kwa muhusiano yake  mazuri  kati ya nchi  yetu ya Tanzania  na  Nchi nyingine  Duniani  hali ambayo imepelekea nchi yetu ya Tanzania kuonekana  kuwa sehemu salama kwaajiliya uwekezaji kwenye sekta ya Madini.

Ameeleza   kuwa Rais Dkt  Samia  Suluhu Hassani  ameleta fedha nyingi kiasi cha shilingi Bilioni 158 kwa ajiri ya shughuli mbalimbali za mendeleo na kuboresha miundo mbinu   hali ambayo imekuwa ni kivutio kwa wageni mbalimbali   kufika katika Wilaya ya Mpanda .

Amefafanua kuwa sekta ya madini ni sekta inayokua kwa kasi sana  katika Wilaya ya Mpanda  ambayo imekuwa inakuwa kila siku  na imekuwa ikipokea wawekezaji wengi  kutoka nje ya wilaya na   nje nchi kwa ajiri  ya uwekezaji .

Mwandisi  Alex   Mwidunda  kutoka  kutoka ofisi ya  Afisa  madini  Mkazi   Katavi amesema  kuwa  madini ambayo yanapatikana  Katavi yapo ya aina sita ambayo ni  Dhahabu ,Shaba , Galena ,Mica (ulanga) madini ya ujenzi na mika .

Amesema  wachimbaji wa madini wa Mkoa wa Katavi wanakabiliwa na changamoto mbalimbali  baadhi ya changamoto hizo  ni ukosefu  wa uwelewa  juu  ya  masuala   mbalimbali ya sheria za  madini.

Mchimbaji   mdogo wa  madi ya dhahabu George Kalasi ameiomba serikali iona namna ya kuweza kuwasaidia wachimbaji kwa kuwapunguzia baadhi ya kodi za tozo.   

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages