ASKOFU WA AWAOMBA WANANCHI KULINDA AMANI NA UTULIVU WAKATI WA PASAKA

Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi ya ziwa Tanganyika Imani Kibona akitoa neno kwa wageni walioshriki hafla hiyo.

 Na Walter Mguluchma-Katavi

Askofu wa  Kanisa  la KKKT   Dayosisi  ya Ziwa Tanganyika  Askofu  Iman Kibona  wananchi  wa Mkoa wa Katavi  wadumishe  amani wakati wa kipindi cha sikukuu ya pasaka   na baada ya pasaka  kwani wanapaswa watambue   kuwa amani   ni tunu imetoka kwa Mungu .


Askofu wa  Kanisa  la KKKT   Dayosisi  ya Ziwa Tanganyika  Askofu  Iman Kibona  wananchi  wa Mkoa wa Katavi  wadumishe  amani wakati wa kipindi cha sikukuu ya pasaka   na baada ya pasaka  kwani wanapaswa watambue   kuwa amani   ni tunu imetoka kwa Mungu .

Wito huu ameutowa  wakati kati wa  hafla ya chakula  cha jioni  iliyoandaliwa  Dayosisi  ya  Ziwa  Tanganyika  Ushirika  wa  Nazareth  Mpanda  kwa ajiri ya kuchangia ujenzi wa  makazi  ya nyumba ya  mchungaji wa  ushirika huo na  mgeni Rasmi alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi aliyewakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika  Onosmo Buswelu .

Amesema amani ni tunu  ambayo tumepewa na Mungu   hivyo anawasihi sana waumi na wasio waumini  washerekee sikukuu ya Pasaka  wakiwa wanadumisha amani kwenye familia zao kwani amani ya kwanza inaanzia kwenye familia .

Amebainisha kuwa familia ikiwa na amani waumini na wasio waumini wanakuwa na amani  na hivyo watakuwa wanadumisha amani kwenye maeneo wanayoishi .

Askofu Kibona  amewasisitiza wananchi  wailinde na kuitunza amani ya nchi yetu kwani inategemewa kulindwa na watu wenyewe   na ndipo tunapo weza kukaa kama ambavyo tunavyoishi sasa    kwenye nchi  nyingine hali sio nzuri  na tunapo ona hivyo tusifurahie  bali  na wao tuwaombea .

Katika hotuba yake Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Mwanavua Mrindoko  iliyotolewa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu amesema  Serikali ya  Mkoa wa KatavI  wanayo  nia ya dhati kabisa  inayoongozwa  na Rais   Dkt  Samia  Suluhu  Hassan  kuwaelekeza viongozi wote wa serikali  kufanya kazi  kwa  kushirikiana na madhehebu yote  ya dini .

Aidha  Mkuu wa Mkoa wa Katavi amewaomba viogozi wote wa dini  wapande miti ya matunda kwenye maeneoyao yao  yanayozunguka nyumba zao za ibada na wanayomiliki  ili  kuweza kupata matunda yatakayosaidia kukabiliana na hali ya udumavu katika Mkoa huu.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages