![]() |
| Kaimu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi Stewart Kiondo |
Na Walter Mguluchuma
Katavi .
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Katavi wamefanikiwa kuokoa kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 29 kufatia kazi walizofanya kwa kipindi cha miezi mitatu za kuzuia Rushwa na uchunguzi .
Hayo yameelezwa na Kaimu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi Stewart Kiondo wakati alipokuwa akitowa taarifa ya utendaji wa taasisi hiyo mbele ya wandishi wa Habari ya kipindi cha miezi mitatu kuanzia mwezi Oktoba hadi Desemba 2025 kwa niaba ya Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi .
Amebainisha kuwa Takukuru Mkoa wa Katavi katika kipindi hicho cha miezi mitatu ya utendaji wao wa kazi wameweza kuokoa kiasi cha tsh 29,994 ,982kupitia kazi za uzuiaji wa Rushwa uchunguzi na kusaidia kuongezeka kwa mapato ya Halmashauri .
Amebainisha kuwa tshs 12,000,000 zimerejeshwa baada ya kubainika nikopo ya asimilia 10 iliyotolewa na Halmashauri ya Mpimbwe kwa kikundi cha wanawake ilitumika kwa matumizi yasiyokusudiwa kufatia ufatiliaji wa Takukuru fedha hizo zilirudishwa na kuwekwa kwenye akaunti ya Wanawake ,vijana na watu wenye ulemavu .
Kiondo amesema tshs 17,994,982 zimerejeshwa kupitia hatua za uchunguzi na mashitaka baada ya washitakiwa katika mashauri mbalimbali kuingia makubaliano ya kisheria (plea Bargaining) fedha ambazo zilihusisha mapato ya ndani yalikusanywa kupitia mfumo wa POS na aziwekwa Benki kwa ajiri ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlele na zilikuwa zimetumiwa kwa matumizi yasiyokusudiwa .
Kuhusu malalamiko kwa kipindi hicho wameweza kupokea jumla ya malalako 32 kati ya malalamiko hayo 17 yalihusu tuhuma za Rushwa na yaneandelea na uchunguzi ambapo malalamiko 15 hayakuhusu tuhuma za Rushwa na walalamikaji walishauriwa na kuekekezwa sehemu sahihi ya kupeleka .
Kiondo amesema Takukuru Mkoa wa Katavi wameweza kushinda kesi tatu walizopeleka Mahakamani na wamefungua kesi mpya mbili huku kesi 10 zikiwa zinaendelea kusukilizwa Mahakamani zikiwa zimesikia hatua mbalimbali .

