MKUU WA WILAYA MPANDA AMSHUKURU RAIS DK.SAMIA

 

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph


Na  Walter Mguluchuma, Katavi.

Mkuu wa Wilaya ya  Mpanda Mkoa wa Katavi  Jamira Yusuph ametowa shukurani za dhati  kwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa Wilaya ya Mpanda  kwa namna ambavyo Rais ameendelee kuwaletea fedha nyingi  kwa ajiri ya utelezaji wa  shughuli mbalimbali za Maendeleo.





Jamila ametowa shukurani hizi  wakati alipokuwa akiwahutubia wajumbe wa mkutano wa Kamati ya ushauri ya Wilaya ya Mpanda (DCC) kwenye kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda.

Amebainisha kuwa hata wajumbe wa kikao hicho watakuwa ni mashahidi kwa fedha nyingi za utekeleza wa shughuli za maendeleo  zilizopelekwa katika Wilaya ya Mpanda kwani  kwa mwaka huu wa fedha Halmashauri ya Nsimbo wameisha pokea   kiasi cha  Shilingi   bilioni  14 na Manispaa wamepokea bilioni 16 ambazo  zimeenda  kwenye shughuli za maendeleo na majeti hiyo bado inaendelea.


Mzee Vicent Nkana akichangia mada katika kikao cha DCC



Amesema  kwa mwaka wa fedha ujao wa 2026/2027 bajeti za Halmashauri  mbili zilizopo latika Wilaya ya Mpanda zimeongezeka  kwa mfano Manispa ya Mpanda Bajeti iliyopita ilikuwa ni bilioni 33.9 lakini bajeti ijayo ni Bilioni  35.2na Nsimbo ilikuwa  Bilioni 27.4 bajeti ijayo  ni Bilioni 35.7 na pia kwenye Taasisi  nyingine   za Serikali bajeti imeongezeka.

 Dc  Jamila  ameeleza kuwa  kwenye  mapato ya ndani pia yameingezeka  kwa Halmashauri zote mbili mwaka  wa  fedha uliopita mapato ya ndani ilikuwa ni Bilioni  6.7  kwa  bajeti ijayo  mapato ya ndani ni bilioni 7.5 mbali ya bajeti fungiwa ongezeko hilo  ni matumaini makubwa kwa wananchi wa Wilaya ya Mpanda  kama ilivyo dhamira ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ya kuwaletea Maendele wananchi .

Mzee maarufu wa Wilaya ya Mpanda Vicenti Nkana  amewapongeza  viongozi wa Wilaya ya Mpanda  kwa kuwa wamekuwa ni watu  wa kwanza  kugundua makosa yanapokuwa yametokea na  kuyafanyia kazi mapema na kutatua.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages