KAMPUNI YA  PREMIUM YATOWA DAWATI 300 KWA WILAYA YA TANGANYIKA

 

Na Walter Mguluchuma, Katavi.

Kampuni ya ununuzi wa zao la Tumbaku PREMIUM ACTIVE TANZANIA  imetowa  dawati 300 zenye  thamani ya Zaidi ya shilingi  Milioni 29 kwa  Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika  kwenye maeneo yanayolima zao la tumbaku  ikiwa ni mchango wa maendeleo ya jamii kwenye maeneo yanayo lima tumbaku kwenye Halmashauri hiyo katika  kuunga  mkono jitahada za serikali  za  kuboresha  sekta ya elimu  hapa Nchini.


Meneja Shughuli  wa Kampuni ya Premium  ACTIVE  Tanzania Nico Roussos amekabidhi mchango huo wa maendeleo kwa jamii mawati  300 kwa Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika  Onesmo Buswelu
Roussous amebainisha kuwa lengo la kukabidhi  dawati hizo 300  ni mchango wa Kampuni ya PREMIUM Active Tanzania   ni kwa ajiri ya kusaidia  kwa kurudisha faida  sehemu  ya faida  inayopatikana  kwa wabia wao  wao  wakulima wa tumbaku ambao ni wananchi wa wilaya ya Tanganyika.

Amesesema  katika kufanikisha zoezi hilo la kurudisha sehemu ya faida  inayopatikana kampuni  hupokea  kipaumbele cha mahitaji kutoka katika sehemu husika  kwenye maeneo ya  Kata zenye  vyama vya  ushirika  vya msingi  vinavyofanya kazi  na Kampuni ya premium.

 Kwa Mkoa wa Katavi walipokea maombi  ya kutengenezwa madawati 753 yenye thamani ya  shilingi milioni tshs  77,990,576.22 kati ya madawati hayo Wilaya ya Tanganyika wao wamepewa madawati 300 kwa ajiri ya shule za awali na msingi .
Roussous amefanunua kuwa   kwa mwaka  2026 kampuni ya Premium  Active  inatowa  mchango  wa maendeleo  ya jamii  kwa Halmashauri  za Wilaya nane hapa nchini  ambapo  wamechangia madawati  kwa shule za msingi na sekondari Pamoja na  vifaa vya  ujenzi ,michezo mbalimbali   ambapo jumla ya thamani  yote ikiwa ni Tshs 162,832,737.06






Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu  wanaipongeza kampuni ya Premium kwa kumuunga mkono  Rais Dkt Samia Suluhu Hassan  katika kuchangia  mahitaji  katika sekta ya elimu hapa nchini.

Amewaomba wadau wengine wainge mfano  wa kampuni hiyo katika kugusa mahitaji  ya Watanzania  na wameisha jipanga kuhakikisha kila dawati linafika haraka sana kwenye eneo usika siku  hiyo hiyo.

Buswelu amesema kwa namna nyingine wanafunzi watakao yakalia  madawati hayo wazazi wao ni wakulima wa tumbaku hivyo  watafahamu kuwa kampuni ya Premium imewachangia madawati  wataendelea kukumbuka kuwa kilimo cha tumbaku  pia kinaleta  madawati.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Tanganyika Shabani Juma  amesema  madawati hayo yatawasaidia kupunguza tatizo la upungufu wa madawati  wao pia kama Halmashauri wanazo pia  juhudi  za utengenezaji wa madawati na wameisha  wameisha towa tenda  ya  kutengeneza madawati 3,600

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages