UVCCM TANGANYIKA WANUFAIKA NA MAFUNZO TRA

Mwenyekiti mstaafu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Kada wa chama  hicho Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi,Ndg Method Mtepa akiendesha mafunzo maalumu kwa vijana wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM) wilaya Tanaganyika.  

 
Na George Mwigulu KTPC,Tanganyika.

Kupitia Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi,Vijana wamenufaika na mafunzo ya mlipa kodi  na ushuru mbalimbali yaliyotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) mkoani humo ili kuwajengea uzalendo kwa taifa na kuwajibika kulipa kodi.

Mafunzo hayo yametolewa na TRA wakati wa kuelekea maadhimisho ya siku ya kuzaliwa kwa chama cha Mapinduzi (CCM),ambapo kabla ya kilele kitakachofanyika  5,Feb mwaka huu kumefanyika semina maalumu ya kiitikadi  kwa umoja wa vijana hao wilayani Tanganyika.

Emmanuel Msava,Afsa huduma na elimu kwa walipa kodi wa mamlaka ya mapato (TRA) Mkoa wa Katavi akitoa mafunzo hayo jana kwenye semina ya kiitikadi katika ukumbi wa shule ya sekondari Kakoso ameeleza kuwa  walipa kodi wanapaswa kupewa elimu pamoja na mamlaka hiyo kuwa na wajibu wa kuhakikisha walipa kodi  wanapata huduma kwa kiwango cha juu ambacho  serikali imepanga kukitoa.

Afsa huduma na elimu kwa walipa kodi wa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Katavi Ndg Emmanuel Msava akiendelea kutoa elimu kwa vijana wa umoja wa vijana UVCCM Wilaya ya Tanganyika katika shule ya Sekondari Kakoso.

Afsa huduma huyo amefafanua kuwa licha ya mlipakodi anapaswa kusajiliwa na kupewa TIN namba ambayo inamwezesha kupitia biashara yake anayoifanya kulipa kodi pia anapaswa kulipa kodi kikamilifu kinyume na baadhi ya wafanya biashara kuona pekee umuhimu wa kuwa na TIN huku wakikwepa kulipa kodi.

‘’ lengo la kusajiliwa na kupewa TIN namba ni kuwa mfanyabiashara unapaswa kulipa kodi na kama mwananchi unapaswa kuhakikisha kuwa kodi hiyo inaingia serikalini kwa kuomba listi pale unaponunua bidhaa’’ alisema Msava.

Akiwafundisha nani anapaswa kulipa kodi  na umuhimu wa kulipa kodi alisema kuwa  kodi inatokana na vyanzo vitatu ambavyo ni ajira,biashara pamoja na uwekezaji ambapo aina ya kodi hii inatozwa kwa mamlaka ya sheria ya kodi ya mapato.

Baadhi ya vijana waliojitokeza katika shule ya sekondari Kakoso Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi katika mafunzo maalumu ya semina ya kiitikadi kuelekea maaadhimisho ya kuzaliwa chama cha mapinduzi (CCM) kitaifa.


Umuhimu wake ni kusaidia uchumi wa taifa kupanda na kusaidia katika kuendesha shughuli nyingi za kitaifa.

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Tanganyika  Mkoa wa Katavi David Mussolin amesema mafunzo hayo ya kiitikadi yanatokana na maelekezo waliyopewa kutoka makao makuu ya chama hicho ili kuhakikisha vijana wanajengewa uwezo wa kiitikadi na imani ya chama pamoja na mambo mengine.

Mussolin  amesema kuwa mafunzo hayo ya kiitikadi na imani yatawawezesha vijana kuwa na juhudi za kuelewa,kuieleza ,kuitetea na  kuitekeleza itikadi ya CCM.

Vijana wa\ Chama Cha Mapinduzi wakiwa katika hali ya utulivu wakisikiliza kwa umakini mafunzo maalumu ya kiitikadi na imani kwa chama chao.

Awe kijana ambaye siku zote yuko mstari wa mbele katika utekelezaji wa mambo ya uanachana ,sera,miongozo ,kanuni ya UVCCM na katiba ya CCM.

Aidha kuwawezesha vijana kuwa wanaoheshimu watu mwenye tabia nzuri ,muaminifu ,muadilifu mwenye kauli na vitendo vizuri mbele ya jamii huku asiyetoa wala kupokea rushwa au mapato mengine ya kificho.



Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wila\ya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi,Ndg David Mussolin akizungumza na vijana kuhusu umuhimu wa kuwa wazalendo katika kulitumikia taifa.


Secilia Samweli Mkazi wa  kata ya Isengule wilayani humo ambaye ni mshiriki wa mafunzo hayo ya kiitikadi  ameshukuru chama kwa kuandaa mafunzo hayo kwani moja ya mambo alikuwa hana ufahamu nayo ni kuhusu umuhimu wa kulipa kodi.

Hivyo amebainisha kuwa kwa sasa amefahamu kwa upana zaidi namna ambavyo inampasa kuwa balozi wa TRA katika kuelimisha watu umuhimu wa kulipa kodi pamoja na kudai lisiti baada ya kununua bidhaa.

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Kata ya Isengule Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi,Ms Secilia Samweli.


Vilevile amesema kuwa mafunzo ya mada mbalimbali ya kiitikadi na imani kwa chama chake yamemwongezea nguvu ya kuwezo wa  kukitetea  na kukielezea chama kwa ufasaha zaidi.



Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages