MBUNGE KAPUFI AWAPATIA MSAADA WALIOPATWA NA JANGA LA MVUA YUPO MZEE WA MIAKA (84)

 

Mbunge wa jimbo la Mpanda mjini,Sebastian Kapufi(wa pili kulia) akimpatia fedha Tasilimu 600,000/= kwa ajili ya kununulia bati ya kuenzekea nyumba yake iliyo ezuliwa na mvua kali ya upepo na mawe.


Na Walter Nguluchuma KTPC,Katavi.

Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini Sebastian  Kapufi amewapatia msaada wakazi wa Kata ya Ilembo ambao nyumba zao 62 zilienzuriwa na mvua iliyoambana na upepo mkali  na kusababisha nyumba 62 kuenzuriwa    na nyingine kuanguka hari ambayo   imesababisha familia za watu 17  kukosa  kabisa makazi ya kuishi akiwepo mzee wa (84)

 Mvua hiyo ambayo iliyoleta maafa hayo ilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita katika maeneo ya Mtaa wa Ilembo na Mapinduzi katika Kata ya Ilembo Manispaa ya Mpanda .

Hari hiyo imemlazimu Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini  Sebastiani  Kapufi kufanya ziara  kwenye eneo hilo na kuwapatia misaada wahanga hao kulingana na mahitaji yao ya haraka .

 Miongoni mwa wakazi wa Kata hiyo Mzee  Victoria  mfinula (84) alisema kuwa toka nyumba yake ilipoenzuriwa na mvua hiyo iliyoambatana na upepo  pamoja na mawe ya mvua  amekuwa hana makazi ya kuishi .

  Hivyo kwa sasa yeye na mke wake ambao wote ni wazee kutokana na umri wao kuwa mkubwa  na kuwa  na  kipato kidogo  hawana uwezo tena wa kurejesha paa la nyumba yao ambayo ilikuwa imeenzuka  paa lake lote na ipo hatarini kuanguka kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha . 

 Mbunge Kapufi kutokana  na hali ambayo alikuwa  nayo mzee huyo na familia yake alionekana kushitushwa na mazingira ya mzee huyo na ndipo alipowauliza wafundi waliokuwepo hapo  gharama ya ujenzi wa paa la nyumba hiyo pamoja na bati unagharimu  kiasi gani alijibu kuwa ni kiasi cha Tshs 600,000.

Baada ya  kuambiwa kiasi hicho cha fedha alimkabidhi mzee huyo na kuagiza ujenzi wa paa ya nyumba hiyo ufanyike haraka sana  hari hiyo ilimfanya mzee Victoria  Mfinula alitowe shukurani kwa Kapufi na kutamka kuwa amemtowa kwenye shimo la kaburi kwani alijua kuwa nyumba yake haita pona tene .

 Akilelezea hari ya tukio hilo   Mkazi wa Mtaa wa Ilembo  Evaristi Salinga  alieleza kuwa mvua hiyo ilianza majira ya alfajiri  huku ikiwa  upepo  mkali na radi za mara kwa mara  na mvua ambayo  ilikuwa inaangusha barafu kama mawe makubwa ambayo yamefanya uharibifu wa mazao na hasa mahindi .

 Nae  Jremia Bwilo  alisema  mvua hiyo ilianza saa kumi na mbili alfajiri  na wakati akiwa ndani ya nyumba yake yeye na mke wake na watoto watatu  wakiwa bado wamelala  ambayo imeanguka  aliona upepo mkali  na mvua ya mawe  na kisha aliona paa ya nyumba yake likienzuruliwa  na kisha aliona ameangukiwa na matofali ya nyumba yake yaliomfanya apate majeraha kwenye mwili wake na bado anaendelea na matibabu .

 Afisa  Mtendaji wa Kata ya Ilembo  Elimili  Katendele  alisema kuwa kwenye tukio hilo  nyumba 62 zimeenzuliwa  huku Kaya 17 zikiwa zimekosa makazi kabisa na wamehifadhiwa  kwa majirani zao .

  Alitaja sababu kubwa kwa kutokea kwa maafa hayo licha ya kuwa mvua ilikuwa ni kubwa iliyokuwa imeambatana na upepo ni wakazi wa eneo hilo kujenga nyumba zao bila  kuwa na lenta .

  Sababu nyingine  ni  eneo hilo kutokuwa  na miti hari ambayo inafanya kuwa wazi na upepo kusambaa kwa urais .

Katentele alieleza kuwa kwenye ziara hiyo Mbunge huyo aliwatembelea wahanga wote 62 na aliweza kuwapatia kila mmoja fedha kadri ya mahitaji yao ingawa aliwaambia  anajua wengine azitawatoleleza  na  wale walioumia  aliweza kuwapatia fedha za matibabu   fedha hizo ni zaidi ya milioni nane 

 Kwa upande wake Mbunge Kapufi alisema yeye mwenyewe ameweza kufika kwenye eneo hilo na kujionea kwa macho matatizo ya wananchi hao .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages