KATAVI YATOWA TAMKO LA KUSHITUSHWA NA KIFO CHA MAGUFULI




Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Katavi ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Mpanda.
Na  Walter  Mguluchuma KTPC,Katavi .

Wakazi wa Mkoa wa Katavi wametowa tamko  la kupokea  kwa mshituko  mkubwa  wa  kifo  cha  Rais  Dkt John Pombe   Joseph  Magufuli  kwa upande  wa  Wanakatavi  ni  Rais  ambae  ameacha  alama kubwa  na isiyofutika  mioyoni  mwa  Wanakatavi  kwa ujumla  wanamkumbuka kwa ujasili  wake  ,uzalendo  na upendo mkubwa  alioonyesha  ni mfano wa  kuigwa  na kama wanakatavi  wanalodeni   kubwa sana  la kuenzi  mazuri yote  
Wakazi wa Mkoa wa Katavi wametowa tamko  la kupokea  kwa mshituko  mkubwa  wa  kifo  cha  Rais  Dkt John Pombe   Joseph  Magufuli  kwa upande  wa  Wanakatavi  ni  Rais  ambae  ameacha  alama kubwa  na isiyofutika  mioyoni  mwa  Wanakatavi  kwa ujumla  wanamkumbuka kwa ujasili  wake  ,uzalendo  na upendo mkubwa  alioonyesha  ni mfano wa  kuigwa  na kama wanakatavi  wanalodeni   kubwa sana  la kuenzi  mazuri yote  

Tamko hilo la wananchi wa  Mkoa wa Katavi  limetolewa kwa niaba yao  na  Mkuu wa  Mkoa wa  Katavi Juma  Zuberi  Homera  katika tamko lililotolewa kwa niaba yake na   Mkuu wa  Wilaya ya  Mpanda Jamira  Yusuph ambae aliagua kilio  na kutokwa   machozi wakati akisoma taarifa hiyo.

Amesema  anaposema  kuwa    Rais  John  Magufuli  aliwapenda wana Katavi  lazima  kuvuta kumbukumbu  ya Katavi  ya mwaka 2015 kabla  ya kuingia  madarakani  na  leo  anapowaacha  wakiwa 2021.


Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi ambaye pia ni Mganga Mkuu wa mkoa huo,Dkt Omary Sukari
Mkoa huu umetengenezewa  barabara  za kiwango cha lami  kutoka  Mpanda kwenda Tabora  ambapo ujenzi wake upo karibu kukamilika  muda si mrefu , Mpanda  kwenda Uvinza  na  Sumbawanga  hadi Mpanda  ambazo  zinafanya kazi  na kuwa  kitovu   cha uchumi  wa Mikoa  ya Rukwa , Kigoma  na  Tabora .

Pia uimarishaji  wa safari  za gari moshi  ya  Tabora     hadi Mpanda  Katavi  pamoja na mpango wa ujenzi wa reli ya kisasa  standard  gage  Mpanda  kuelekea  Karema  ambayo  ujenzi  wake  unaendelea  na uwanzishwaji wa safari za ndege   kwa waki mara  na safari hizo za ndege alifungua yeye  mwenyewe  Rais  Magufuli  alipofanya  ziara  Mkoani Katavi  mnamo  tarehe  12  Oktoba 2019. 
Aidha kwa kutambua  kuwa  Mkoa wa Katavi  ni wenye uzalishaji  mkubwa  ameelekeza  kuunganishwa na  Grid  ya Taifa  na ujenzi wa miundo  mbinu  hiyo  inakamilishwa  oktoba  2021 sambamba na usambazaji  wa umeme  wa REA  ambapo  mwanga umewafikia wananchi  kwa asilimia 90 hadi sasa. 
Homera amesema  watakuwa wachoyo wa   fadhila  kama   wasipokumbuka  alivyowajali  wanyonge  wa Katavi  kama  alivyosisitiza  kuwa yeye  ni  Rais wa wanyonge  kwa kuboresha  huduma za jamii hasa katika  Afya   ,elimu na  Maji  wote watakuwa  watakuwa mashahidi  kuwa wamefaika na elimu ya msingi na Sekondari bila malipo  ujenzi  wa vituo  vya afya katika Mkoa huo  vinane  vinavyotowa huduma kwa sasa na Hospitali  nne za Wilaya  na  Hospitali moja ya Rufaa ya Mkoa.
Ameeleza  hakika atakumbukwa  sana  hasa na akina mama  ambao  walikuwa wanakumbwa  na adha ya upatikanaji  wa maji  katika  familia zao  na hata  kupelekea  ndoa kuvunjika .

Ametowa  rai  kwa wananchi wa wa Mkoa wa  kuendelea kuwa  watulivu  wastahimivu  na kuendelea kuimarisha upendo ,mshikamano  ,undugu  na umoja  hasa katika  kipindi  hiki kigumu  huku wakimwombea  heri  mbele za Mwenyezi  Mungu  apumzike kwa amani.

 

 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages