![]() |
Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Katavi,Christopher Nakua. |
Na George Mwigulu,Mpanda
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Katavi kwa kipindi cha miezi mitatu ya kuanzia Januari mwaka huu hadi Machi wamepokea malalamiko 80 kati ya hayo 26 yalihusu vitendo vya Rushwa.

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Katavi kwa kipindi cha miezi mitatu ya kuanzia Januari mwaka huu hadi Machi wamepokea malalamiko 80 kati ya hayo 26 yalihusu vitendo vya Rushwa .
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Takukuru wa Mkoa wa Katavi Cristopher Nakua wakati alipokuwa taarifa kwa umma mbele ya wandishi wa Habari juu ya utendaji kazi wa Taasisi hiyo kwa Mkoa wa Katavi kwa kipindi cha januari hadi Machi 2021.
Alisema katika kipindi cha Januari hadi hadi Machi wamepokea jumla ya malalamiko 80 kati ya hayo malalamiko 26 yalihusu vitendo vya Rushwa na malalamiko 54 yalihusu makosa mengine .
Katika kipindi hicho majalada matatu yalipelekwa kwa DPP, kesi mbili zilifunguliwa Mahakamani ambapo kwenye kipindi hicho kesi moja iliamuliwa Mahakamani na watuhumiwa wote katika kesi hiyo walitiwa hatiani na kuhukumiwa vifungo au faini.
Nakua alizitaja kesi hizo zilizofunguliwa Mahakamani kesi ya kwanza ni CC.18/2021 ambapo Februari 10 mwaka huu Takukuru Mkoa wa Katavi walimfikisha Mahakamani Pridance Anacredo pamoja Varanto Gattaro ambao walikuwa viongozi wa Amcos Mishamo kwa kosa la kutumia vibaya madaraka ya ofisi kinyume na kifungu cha sheria cha 31.
Aliitaja kesi ya pili ni kesi ni kesi yenye Namba ECC.01/2021 ambapo mnamo tarehe 12 Februari 2021 walimfikisha Mahakamani katika Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Juma Mnyongalule kwa kosa la kujipatia fedha kiasi kiasi cha Tshs 3,750,000 isivyo halali kwa kuendelea kulipwa na kupokea mshahara kutoka shirika la Reli Tanzania alikokuwa akifanya kazi hapo awali kama fundi mchundo .
Nakua alisema kwa upande wa kuzuia na ufuaatiliaji wa miradi ya maendeleo wamefanya kazi ya uchambuzi wa mfumo kuhusu utoaji wa vibali vya ujenzi nchini katika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda .
Pia wamefanya kazi ya ufatiliaji wa fedha za Miradi ya Maendeleo ambapo miradi kwa kufatilia miradi inayohusiana na mfuko wa Mandeleo ya Jamii awamu ya tatu TASAF kwenye Wilaya ya Mpanda .
Ufatiliaji huu wameufanya kwenye Kata za Kawajense , Makanyagio ,Kazima , Nsemlwa na Ilembo uliokuwa na thamani ya Tsh.26,000,000 `` Alisema Nakua .