TAKUKURU MKOA WA KATAVI WAOKOA ZAIDI YA MILIONI 132.


Na Walter Mguluchuma KTPC,Katavi

 Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Katavi imefanikiwa kuokoa zaidi ya milioni 32 fedha hizo  ni zile  ambazo  zilikuwa  zichepushwe au kufanyiwa  ubadilifu  kinyume  na sheria  ya kuzuia  na kupambana na Rushwa  Na  11 ya mwaka 2007.



Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Katavi,Christopher Nakua.

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Katavi imefanikiwa kuokoa zaidi ya milioni 32 fedha hizo  ni zile  ambazo  zilikuwa  zichepushwe au kufanyiwa  ubadilifu  kinyume  na sheria  ya kuzuia  na kupambana na Rushwa  Na  11 ya mwaka 2007.

 Hayo yalisemwa na Mkuu wa Takukuru wa Mkoa wa Katavi Cristopher  Nakua alipokuwa akitowa taarifa ya utendaji kazi wa Taasisi hiyo kwa kipindi cha kuanzia mwezi Januari mwaka huu hadi mwezi machi mbele ya Wandishi wa Habari .

 Alisema  katika kipindi cha mwezi Januari hadi hadi  Machi mwaka huu Takukuru  Mkoa wa Katavi  katika uchunguzi waliofanya  kupitia   operesheni  mbalimbali walizofanya  wameweza kufanikiwa kuokoa  jumla ya  Tsh,132,172,246 ambazo  zilikuwa zichepushwe na kufanyiwa ubadilifu .

 Nakua  alibainisha kuwa   kati ya fedha hizo  kiasi cha  Tshs  250,000 zimeokolewa kutoka  Mpate  Saccos Tsh, 3233,000 zmeokolewa kutoka  Manispaa ya Mpanda ambazo zimetokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani fedha hizo azikuwa zimetumika kama alivyokusudiwa kwa wa ajiri ya mkopo wa vijana ,wanawake na wenye ulemavu .

 Fedha nyingine zilizookolewa ni fedha  za ukusanyaji  wa ushuru  kwa njia ya  kieletroniki (pos)  tsh ,68,186,246. na kiasi cha Tsh 5,503,950 zimerejeshwa ikiwa ni malipo ya wakulima wa pamba  ambazo zilikuwa kwenye kiwanda cha  NGS.

 Alifafanua kuwa  fedha zilizorejeshwa kwa wananchi  binafsi  ni kiasi cha tsh milioni ,85.4 akiwemo mwalimu  mstaafu  Geoge  Kanyukamamalunde  aliyekuwa amedhurumiwa  fedha mafao yake ya kustaafu .

 Katika kipindi hicho  katika kutekeleza  jukumu lao  la kuelimisha jamii na kuhakikisha  umma  katika mapambana dhifdi ya rushwa TAKUKURU Mkoa wa Katavi wametoa semina sita kwa makundi manne tofauti juu ya madhara ya rushwa na utendaji kazi wa TAKUKURU na onesho moja pamoja na makala nne.

Mkakati wa kipindi cha  pili kutoka April hadi June wanatarajia kuongeza nguvu katika uchunguzi wa malalamiko yanayopokelewa hasa ubadhirifu wa fedha kwenye vyama vya ushirika.

Pia taarifa za ukaguzi wa mahesabu za halmashauri zote na pia kutoa elimu jwa wananchi pamoja na kushughurikia malalamiko mbalimbali ya wananachi yanyohusiana na rushwa kupitia TAKUKURU inayotembea.

Nakua alitowa shukrani kwa wanahabari kwa ushirikiano wao mkubwa katika mapambanon dhidi ya rushwa na anawaomba wandeleze mapambano hayo dhidi ya rushwa.


Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages