Na Walter Mguluchuma KTPC,Mpanda.

Badhi ya Mabalozi wa CCM katika Kata ya Nsemlwa Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wametishia kujiondoa katika nyadhifa zao za uongozi wa shina( BgALOZI) kwa kile wanachodai kuwa wamekataliwa kuwa wanufaika wa Mpango wa kuzinusu Kaya masini Tasaf wakati wao hawapati ruzuku yoyote ya kutoka kwenye chama chao na hali ya maisha yao yako duni .
Mabalozi hao wametowa kauli hiyo hapo Mei 30 kwenye kikao cha kuwatambua walengwa wa Kaya maskini kilichofanyika katika Mtaa wa Migazini Kata ya Nsemlwa na kuleta mtaafaruku mkubwa kwenye mkutano huo
MMoja wa viongozi hao ambae ni Katibu wa Kata wa CCM wa Kata ya Nsemlwa Charles Maganga alisema kitendo cha kusomewa vigezo vya watu ambao wanatakiwa kujiunga kwenye mpango wa Tasaf hauja wafurahisha mabalozi ambao wametishia kujiondoa kwenye nafasi hiyo baada ya kuambiwa kuwa wao hawana sifa za kuwa kwenye mpango wa Kaya maskini .
Alisema kwenye mpango huu wamesomewa sharti ambalo linawaondoa viongozi wote wa vyama, dini na wale wa Serikali bila kuwa wameangalia hali zao za maisha wakati wao pia maisha yao yako duni sana kimaisha .
Alitaja kigezo kingine walichotajiwa za watu ambao hawana sifa za kuwa kwenye mpango ni mtu ambae ana mtoto ambae anaweza kumuudumia asisaidiwe kuwa mmoja wa wanufaika .
Maganga alisema kuwa watu wanaohitajika kuwa kwenye mpango wameelezwa kuwa ni watu ambao hawana uwezo wa kula milo mitatu kwa siku,watu wenye ulemavu na watu ambao ni maskini sana wa kipato ambao hata wakipata malazi wanakuwa hawana uwezo wa kununua panald alihoji kuwa watu kama hao ambao hawana uwezo wa kununua hata panald moja mbona hawapo wote walicha kufa .
Amebainisha kuwa mabalozi hao wametishia kujiuzuru nafasi ya ubalozi kwa kuwa wamekuwa wakifanya kazi kubwa wakati hawapati ruzuku yoyote ile hivyo ni jema wakajiondoa ili nawao wanufaike na Tasaf .

Mwenyekiti wa Mtaa wa Migazini Ahamad Kahena alisema kuwa mpango ulikuwa unaenda vizuri lakini kutokana na kitendo cha mabalozi kutishia kujiuzuru kumewafanya watu kwenye kikao cha kupendekeza majina watu washindwe kwa makusudi kutaja majina ya walengwa .
Alisema kuwa mabalozi wa ccm hawana mishahara wanayo pata na hata kwa viongozi wa ngazi ya tawi nao ni hivyo hivyo hawapati chochote ndio maana wanataka kujiondoa ili nao wawe wanufaika wa Tasaf .
Mwenyezaji wa Kaya maskini wa kutoka Manispaa ya Mpanda Miliamu Kavua amesema mwitikio wa wananchi kwenye mkutano wa kupendekeza majina ya walengwa umekuwa ni mdogo baada ya mabalozi wa nyumba kumi kutotowa ushiriiano wa kutosha .
Amesema viongozi hao wamekuwa wakilalamika kuwa vigezo vimewaondoa wakati wao hawapati kitu chochote kwenye chama chao .
Hivi karibuni viongozi wa Kata mbalimbali wakiwemo na madiwani walipatiwa mafunzo ya uwelewa wa pamoja juu ya mpango wa Tasaf ili wawezekuwaelisha wananchi waondokane na changamoto ya kutoelewa mpango huu kama awamu iliyopita
Alisema kuwa mabalozi wa ccm hawana mishahara wanayo pata na hata kwa viongozi wa ngazi ya tawi nao ni hivyo hivyo hawapati chochote ndio maana wanataka kujiondoa ili nao wawe wanufaika wa Tasaf .
Mwenyezaji wa Kaya maskini wa kutoka Manispaa ya Mpanda Miliamu Kavua amesema mwitikio wa wananchi kwenye mkutano wa kupendekeza majina ya walengwa umekuwa ni mdogo baada ya mabalozi wa nyumba kumi kutotowa ushiriiano wa kutosha .
Amesema viongozi hao wamekuwa wakilalamika kuwa vigezo vimewaondoa wakati wao hawapati kitu chochote kwenye chama chao .
Hivi karibuni viongozi wa Kata mbalimbali wakiwemo na madiwani walipatiwa mafunzo ya uwelewa wa pamoja juu ya mpango wa Tasaf ili wawezekuwaelisha wananchi waondokane na changamoto ya kutoelewa mpango huu kama awamu iliyopita