RC HOMERA AMELITAKA JESHI LA POLISI KUCHUKUA HATUA DHIDI YA WATOTO WANAOFANYA BIASHARA MITAANI.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Comrade Juma Zuberi Homera.


Na  Walter  Mguluchuma KTPC,Katavi.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Zuberi Homera amemeagiza jeshi la Polisi hukakikisha linawakamata watoto wote wenye umri wa  chini ya miaka 18 watakao onekana wanazurula mitaani na kufanya biashara ndogo ndogo  na kuuza vyuma chakavu  kuwakamata na kuwaweka ndani na wazazi wao wakifike kuwakomboa  na wawekwe ndani ili watowe maelezo kwa nini wanawatuma  watoto wao kufanya biashara  huku wakiwa na umri mdogo.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Zuberi Homera amemeagiza jeshi la Polisi hukakikisha linawakamata watoto wote wenye umri wa  chini ya miaka 18 watakao onekana wanazurula mitaani na kufanya biashara ndogo ndogo  na kuuza vyuma chakavu  kuwakamata na kuwaweka ndani na wazazi wao wakifike kuwakomboa  na wawekwe ndani ili watowe maelezo kwa nini wanawatuma  watoto wao kufanya biashara  huku wakiwa na umri mdogo .

Homera ametowa maagizo hayo  wakati alipokuwa akizungumza na wananchi wa Manispaa ya Mji wa Mpanda .

 Ameagiza kuwa mtoto yoyote yoyote ambae atakae aonekana akifanya biashara za kuuza bidhaa mbalimbali mitaani na kuuza vyuma chakavu    wakamatwe mara moja  na kuwekwa  mahabusu na   endapowazazi wao nao watajitokeza kwa ajiri ya kwenda kuwatowa nao watawekwa ndani na kisha watatakiwa wajieleze ni kwanini wanawatuma watoto wao kwenda kufanya biashara  wakati wakijua kuwa ni watoto   wao wanaumri mdogo .

Akiona tena kwenye meneo ya Mji wa Mpanda watoto wadogo wanaendelea kufanya biashara mitaani bila kukamatwa Mkuu wa  polisi wa Wilaya ya Mpanda ajuwe kuwa  ameshindwa kutimiza agizo la Mkuu wa Mkoa na mkuu huyo wa P olisi (OCD)  atambue kuwa kuanzia siku hiyo atafute kituo kingine cha kufanyia kazi na si kwenye  kwenye Wilaya ya Mpanda.

Amesema Mkoa wa Katavi hauwezi kupata kashifa ya watoto kutokwenda shule na badala yake wanafanya biashara mitaani.

Homera alisema haiwezekani watoto washindwe kwenda shule  na badala yake wanakwenda kuuza vyuma chakavu na fedha hizo wanawapelekea wazazi wao.

Angekuwa na mamlaka angekuwa anawachapa vibokokabla ya kuweka mahabusu lakini polisi sheria hiyo inawaruhusu.

Serikali inaendelea kufanya shughuli za kupeleka maendeleo kwa wananchi  na wao wazazi wanakuwa  na tabia yao ya  kuwatuma watoto wao kufanya biashara ya kuuza mayai.

Kumekuwa na tabia ya badhi ya watu  watu kujifanya kuwa wanataka kununua bidhaa kwa watoto na badala  wamekuwa wakiwaita hadi chumbani na kuwafanyia vitendo vya ubakaji .

Hapa ni mjini haiwezekani kuona watoto wanaendelea kufanya biashara mitaani  watawakamata na wazazi wao watafikishwa Mahakamani.

Nae Mkazi wa Mtaa wa Majengo Josephina Joseph amesema kuwa agizo hilo la Mkuu wa Mkoa amelitowa kwenye wakati sasa kwani kemekuwa na wimbi kubwa katika mji wa Mpanda kwa watoto wadogo kufanya biashara  mitaani muda wa masomo.

Juma Hussein  Mkazi wa Mtaa wa Makanyagio amesema kuwa endapohatua za haraka hazitachukuliwa kuna uwezekano mkubwa wa tatizo la mimba za utotoni zikazidi kuongezeka kwa kasi kubwa.




 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages