CWT IMEIOMBA SERIKALI KUTOWAWEKA WALIMU KWENYE MAKAZI YA WAKIMBIZI MUDA MREFU



Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko( katikati) akiwa na baadhi ya viongozi wa mkoa na kitaifa wa CWT.

Na  Walter    Mguluchuma KTPC,Katavi .

Chama cha Walimu Tanzania (CWT( kimeiomba Serikali  kutowaweke muda mrefu walimu wanaofundisha  Shule za Msingi na Sekondari kwenye maeneo ya Makazi ya Wakimbizi  ili wasizeekee huko  bila kujiandalia mambo mengine ya  kimaisha kama vile kujenga  makazi ya kudumu .



 Ombi hilo ametowa wakati wa mkutano  mkuu wa   sita wa  umoja  wa ujirani mwema  Nyanda za juu kusini( SOHITCO( uliofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi ambao umewashirikisha viongozi wa  cwt   wa kutoka katika Mikoa sita ya Katavi , Rukwa, Songwe,  Mbeya,  Njombe na  Iringa .

Akisoma  Risala ya wasshiriki wa mkutano huo mbele ya mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko katibu wa CWT  Mkoa w Katavi  Nuru  Shenkalwa alisema  kumekuwa na changamoto kwa walimu wanaokuwa wamepangiwa kufanya kazi kwenye vituo vya makazi ya wakimbizi kuweza kujenga makazi yao ya kudumu kutokana na sheria zinazo kataza watu kujenga nyumba za kudumu katika makazi ya wakimbizi yaliko katika Mkoa wa Katavi .

 Hivyo  wanaiomba  Serikali  Walimu walioko  kwenye Shule hizo  watazmwe ili  ili wasikae  muda mrefu  ili wasije  wakazeekea huko  bila kujiandalia  mambo yao  mengine  ya kimaisha  mfamo kujenga makazi

yao  ya kudumu .

 Aidha  alisema kuwa watakuwa wachoyo wa fadhila  kama  hawataishukuru Serikali  kwa kupandisha vyeo vya walimu  katika maeneo yao  hali  hiyo  imeondoa  manung-ununiko ya muda mrefu na kuwarudishia  matumaini mapya .


 Hivyo wanaiomba Serikali  iendelee kufanya hivyo  kila  inapobidi  ili wafanyakazi wasikae muda mrefu  pasipo kupandishwa vyeo  wanaamini wafanya kazi  wasipokuwa na manung-uniko  huitendea haki   falsafa ya kazi  iendelee kwa  kuwa  kazi ni  kipimo  cha utu na kazi ni sehemu ya maisha .

 Mweka  Hazina  Hazina wa CWT  Taifa   Aboubakar   Allawi alieleza kuwa    chama hicho kinaishukuru Serikali kwa hali ambayo inayoendelea sasa ya kuboresha miundo mbinu ya kufanyi  kazi walimu pamoja na makazi yao ya kuishi . PAMOJA

 Alisema kuwa anapenda  kuikumbusha Serikali kushughulikia swala la walimu 66,000 ambao majina yao yalihakikiwa mwaka 2017  kwa ajiri ya kupandishwa madaraja  lakini hadi sasa  swala lao halijashughulikiwa hari ambayo imekuwa ikileta malalamiko ya walimu kwenye chama chao kuanzia kwenye matawi hadi Taifa .

Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Mwanamvua  Mrindoko   alibainisha kuwa Serikali  itaendelea  kutowa ushirikiano  kwa chama cha Walimu Tanzania  na vyama vingine vya wafanyakazi ili viweze kutimiza majukumu yao vizuri .

 Alifafanua kuwa hakuna  sehemu ambapo maendeleo yameonekana  au kufanyika  bila kutaja jina La mwalimu katika kuchangia maendeleo hayo hivyo watambue kuwa wao ni watu muhimu sana na Serikali inawategemea .

 Alisema Serikali imejipanga  kuhakikisha  walimu wote wanaishi kwene mazingira mazuri   na bora  kwani inatambua kuwa bado kuna baadhi ya maeneo wanayoishi sio bora.
 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages