WANAOHUJUMU UJENZI WA BANDARI KAREMA WAKAMATWA.




Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi,Benjamin Kuzaga.

Na Mwandishi Wetu KTPC,Katavi.

Ujenzi wa bandari ya Karema ya kimkakati inayoendelea kujengwa katika wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi itakayotumika kwa ajili ya kusafirishia mizingo na abilia kutoka Tanzania kwenda nchi ya DRC Congo baada ya kukamilika,Ujenzi huo umeanza kuhujumiwa kwa kufanyika wizi wa vifaa mbalimbali.



Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko.

Uhujumi huo umebainika baada ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi kufanya operesheni ya misako na doria  maalumu ya  kudhibiti  mtandao wa wizi  wa rasilimali  za mradi  wa ujenzi  wa  bandari ya Kimkakati ya Karema na kufanikiwa kukamata watuhumiwa 16 wakiwa wameiba mafuta ya diseli  lita 4,100 na nondo  68 na vifaa mbalimbali mali ya kampuni inayojenga bandari hiyo.

Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi,Benjamin Kuzaga amewaambia wandishi wa  habari kuwa watuhumiwa hao walikamatwa huko katika Vijiji vya Karema na Ikola kufuatia msako makali ulifanywa na jeshi hilo.

Amesema kuwa kabla ya kufanyika kwa msako huu mkali jeshi Polisi walipata taarifa juu ya hujuma zinazofanywa za wizi kwenye ujenzi huo wa bandari ya Karema inayotarajiwa kukamika kwa ujenzi wake hapo 6 March 2022.

Baada ya taalifa hizo  kufika kwa jeshi la polisi  walifanya msako mkali  na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa 16 wakiwa  na mafuta aina ya diseli lita 4,100, vipande 58 vya nondo , madumu 118 ya plasitiki ,betri mbili za gari  grisi  kilo saba  na oili  lita 10 vyote  vikiwa  mali ya  Kampuni  ya  XIAMEN ON COING  CONSTRACTION GROUP COMPANY LIMETED inayotekeleza  mradi  wa kimkakati  wa ujenzi wa bandari y a  Karema.




Baadhi ya maduma ya mafuta ya dizeli yaliyoibiwa.

Kamanda Kuzaga amewataja watuhumiwa hao waliokamatwa kuwa ni  Jackson Mathias   Mkazi wa Ikola ,Godfey  Kigongo  ,Joseph Haule  wakazi wa Kijiji cha Karema , Ibrahimu  Simba Mkazi wa Kijiji cha Inyonga , Ayubu   Athuman, Chuki  Wiliam,,Jipala  Nekala , Lusonguye  Kaise , Jacob  Thobias Muse   Enelil Benedictor  w ote wakazi wa Karema .

Ameeleza kuwa  watuhumiwa  wote  wanaendelea kuhojiwa kuhusiana na matukio hayo  ya wizi  na mara  baada ya taratibu  zote  za kiupelelezi  kukamilika  jalada  litafikishwa  katika ofisi  ya Taifa ya mashitaka  Mkoa wa Katavi  kwa hatua zaidi za kisheria.


Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akizungumza na wananchi.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amewaagiza watu wote ambao wamehusika na wizi kwenye mradi huo  wajisalimishe kabla hawaja kamatwa  kwani endapo kama watashindwa kusalimisha mali walioiba  wakikamatwa watachukuliwa  hatua kali ikiwemo kuwekwa mahabusu bila kutoka kwani kosa hilo lina husiana na kuhujumu uchumi.

Amesema kuwa kitendo hicho cha wizi ni aibu kwani mradi huu umewekwa kwa ajiri ya kuwasaidia  badala yake wao ndio wamekuwa watu wanaofanya uhalifu ni aibu  na wala Serikali ya Mkoa haita wavumilia hata kidogo.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages