KATIBU TAWALA KATAVI AHIMIZA WAKULIMA KUCHANGAMKIA FURSA YA FEDHA BILIONI 50 ZA ZAO LA PAMBA.


Katibu Tawala Mkoa wa Katavi, Rodrick Mpogolo

 

Na Mwandishi wetu KTPC,Katavi.

Uzalishaji wa zao la Pamba katika Mkoa wa Katavi bado uko chini hali iliyopelekea mwekezaji wa kiwanda cha pamba kubadili matumizi ya fedha za kununulia zao hilo kwa kuzielekeza kwenye kununua zao la mahidi.

Balozi wa Pa,mba nchini Aggrey Mwanri.

Kwa takwimu uzalishaji wa zao la pamba katika Mkoa wa Katavi kwa msimu wa kilimo wa mwaka 2020/21 ni kg 2,173,399 zimezalishwa na kufanya kiasi hicho kuwa ni kidogo hasa ukizingatia soko la zao hilo liko wazi kupiti mwekezaji wa NGS Investment Co Ltd kilichopo wilaya ya Tanganyika kikiwa na uhitaji wa kg Mil 50 wa zao hilo.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi,Rodrick Mpogolo kwa niamba ya Mkuu wa Mkoa Mwanamvua Mrindoko amesema hayo jana katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda Mkoani hapa wakati wa kufungua kikao cha wadau wa kilimo cha pamba kilicholenga kutoa hamasa na elimu ya kuzingatia uzalishaji wenye tija uliotolewa na bodi ya pamba Tanzania.

Mpogolo amesema kuwa msimu wa maadalizi wa kilimo cha pamba umeanza na zoezi la uhamasishaji wa kutoa elimu kwa mkulima ni muhimu kwa Mkoa kutokana na uzalishaji wa zao hilo kuwa chini kwa kuzingatia takwimu  za kg zaidi ya mil 2 ikiwa ni hasi ya kama Kg mil 47 hadi Kg Mil 48.Ikiwa sawa na kupewa fedha ziko na kushindwa kuzichukua.

Balozi wa pamba nchini,Aggrey Mwanri wakionesha namna ya kupalilia kwa ufanisi ili kuchochea ufanisi 

“ nitoe tu kwa wasitani kama kg 1 ya pamba inauzwa kwa Tsh 1,000/- ukizidisha mara Kg mil 50 ni sawa sawa na bilioni 50  ambazo zinaingia kwenye mkoa wetu,lakini sisi hatujawaada wakulima kuchukua hizo billion 50” Alisema Katibu Tawala.

Amefafanua mkoa bado unatatizo na kinachotakiwa kufanywa na watalamu,bodi ya pamba Tanzania na mwekezaji kuwaunganisha wakulima waingie kwenye kilimo cha pamba cha kisayasi ili wazichukue hizo fedha ziingie katika mifuko yao na kuboresha kipato cha familia na mkoa wa Katavi.

Mpogoli amesema “ nilipata kutembelea kile kiwanda cha NGS,Meneja akaniambia kuwa anazo pesa benki kwa ajili ya kupeleka kwa  wakulima lakini kwa kuwa hakuna pamba sasa amelazimika kuanza kuchukua mahidi…sasa baada ya kukosa anachukua mahidi ya wakulima kitu ambacho hakikupangwa kwa ajili ya mahidi”.

Aidha licha ya kuushukuru wijio wa bodi ya pamba Tanzania kupitia balozi wake Aggrey Mwanri na watalaamu wengine amesema kwenye utekelezaji wa malengo ya kilimo wamefanikiwa kugawa mbegu za pamba kwa msimu mpya wa kilimo wa mwaka 2021/22 na  kutoa wito kwa wataalamu wa sekta hiyo kuingia shambani na kuacha kukaa ofisini na kupunguza kuandika na kwenda kufanya kazi kwa wakulima.

Renatus Luneja,Kaimu Mkurugenzi wa bodi ya pamba Tanzania amesema kapeni hiyo ni utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) yam waka 2020/25 inawataka kuzalisha tani milioni moja za pamba ifikapo mwaka 2025.ili kufikia malengo hayo wameweka mikakati ya kuhamasisha wakulima kuongeza tija kwenye uzalishaji wa zao la pamba.

Ameeleza kuwa sehemu nyingi wakulima huzalisha wastani wa kg 300 za pamba kwa hekali moja ikiwa afadhari kwa mkoa wa Katavi huzalisha wastani wa kg 500 za pamba kwa hekali moja.Hivyo uwezo wa mbegu kwa mujibu wa tafiti angalau wasitani wa kg 1,000 zinatakiwa kuzalishwa kwa hekali moja na kusaidia kufikia malengo ya tani milioni moja kitaifa

“ Katavi ni eneo la kimkakati tutakuwepo kwa siku 14 kutoa elimu,Na kwa mkoa huu mmewekewa malengo ya kuzalisha tani 50,000 za pamba kwa mgawanyo wa tani 25,000 halmashauri ya wilaya ya Tanganyika,Tani 16,000 halmashauri ya Nsimbo,Tani 4,000 halmashauri ya wilaya ya Mlele,Tani 5,000 halmashauri 5,000 manispaa ya Mpanda” alisema Lunneja..

Balozi wa zao la pamba Tanzania,Aggrey Mwanri amesema kuwa pamba ni zao muhimu la biashara ambalo linaliingizia taifa fedha za kigeni na wameendelea kufanya kampeni katika mikoa ya Mwanza,Shinyanga,Simiyu,Geita,Mara na Tabora ambapo wamekuwa wakiwahimiza wakulima kufanya kilimo cha kisayansi.

Mwanri amefafanua kuwa katika utoaji wa elimu wamekuwa wakihimiza utayarishaji mapema wa shamba,kutumia mborea za samadi na virutubisho vingine,kupanda pamba mapema,kupanda kwa mistariii na kwa nafasi maalum,kupanda idadiiii halisi ya mbegu katika kila shimo,Kupunguza miche na kupalilia kwa wakati.

Mambo mengine ni kunyunyuzia madawa kuzuia wadudu  waharibifu kwa kuzingatia athari za kutokunyunyuzia,kuvuna pamba mapema na kuchambua pamoja na kung’oa na kuchoma moto masalia yote ya pamba.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages