BIASHARA ZA VYUMA CHAKAVU MITAANI,MBOGA NA MATUNDA CHANZO WATOTO KUTOKWENDA SHULE MUDA WA MASOMO MANISPAA YA MPANDA

Ikiwa ni siku moja baada ya shule kufunguliwa hapa nchini baadhi ya watoto wakiwa mitaani katika Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wakifanya biashara ya vyuma chakavu badala ya kuwa shuleni ((Picha na Walter Mguluchuma)


Na Walter Mguluchuma

     Katavi

 Pamoja na jitihada kubwa zilizofanywa na Serikali za kujenga jumla ya madarasa 425 Mkoa wa Katavi yaliyotokana na fedha  za Mpango  wa Maendeleo  kwa Ustawi  wa Taifa  na  Mapambano dhidi ya Uviko 19 bado Mkoa huu unakabiliwa  na changamoto ya utoro wa wanafunzi kuto kwenda shule na badala yake wamekuwa wakizurura  mitaani kufanya biashara za vyuma chakavu na biashara ndogo ndogo za kuuza matunda .

Hivyo jitihada kubwa zinahitajika kutatua tatizo hizo kuanzia kwa mzazi na mamlaka za Serikali vinginevyo  tunajiandalia bomu la siku za baadae katika Mkoa huu.

 Wakiongea na mwandishi wa habari hizi  majira ya saa tano na nusu asubuhi wakiwa kwenye harakati zao  kufanya biashara za vyuma chakavu  mmoja wa watoto hao amesema kuwa wamekuwa wakizunguka kwenye mitaa mbalimbali ya Mji wa Manispaa ya Mpanda  kutafuta vyuma chakavu na kisha kwenda kuviuza kwa mfanya biashara mmoja waliyemtaja kwa jina moja la John.

Amebainisha kuwa kilo moja ya vyuma chakavu wamekuwa wakiuza kwa bei ya shilingi mia sita na wamekuwa wakiona biashara hiyo ni ya kawaida kwani wamekuwa hawasumbuliwi na mamlaka yoyote ile ya Serikali.

 Nae mtoto mwingine ambae jina limehifadhiwa amesema kuwa  yeye anaishi Kawajense pamoja na wazazi wake ameona kufanya biashara hiyo ni nzuri kwa kuwa inampatia kipato.


Watoto wakiwa mtaa wa madukani na mfuko mgongoni kusaka vyuma chakavu muda wa shule

"hakuna mtu ambae amekuwa akiniuliza kwanini nafanya biashara hii badala ya kwenda shule ni wewe tuu mwandishi ndio umeniuliza  na tupo wengi tuu tunaofanya biashara hii na hasa mida ya asubuhi na jioni"alisema mtoto huyo

 Nae mkazi wa Makanyagio Paulo Mathias  amesema kuwa tatizo hilo la watoto wadogo kufanya biashara limekuwa sugu Mkoa wa Katavi na hasa Manispaa ya Mpanda  hali inayosababishwa na wazazi kutowajibika kwa malezi ya watoto wao na mamlaka husika kutowajibika kuwachukulia adhabu watoto hao.

Hali hii imekuwa ikisababisha Mkoa wa Katavi kuendelea kuwa na idadi kubwa ya mimba za utotoni kwani watoto wakike wenye umri mdogo nao wamekuwa wakipata  vishawishi  wanapokuwa wakifanya biashara za matunda kama ndizi ,matango karanga  na embe .

 Nae Anna John ameleza kuwa swala la watoto kupata mimba za utotoni halitakwisha  Mkoa wa Katavi kutokana na watoto wadogo wa kike kuruhusiwa kufanya biashara za mitaani,mbona maeneo mengine  Mikoani hakuna hali kama hii au Wakuu  wa  Mikoa na Wilaya  huwa wanatofautiana?ni swali kutoka kwa mwananchi Anna

 Diwani wa Kata ya Majengo Magreti John (Kitunguru) amesema kuna shida ya utekelezaji wa zoezi hilo lipo kwa watendaji wa Mitaa na Kata kwani wamesha pewa maagizo ya kuwakamata watoto  wote wanaofanya biashara za kuuza mboga za majani ,matunda na vyuma chakavu muda wa shule lakini hawafanyi hivyo.

Watoto kutoka eneo la kawajense  Manispaa ya Mpanda wakisaka vyuma chakavu ili kujipatia kipato muda wa masomo.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages