KAMATI YA SIASA MKOA WA KATAVI YAFANYA UKAGUZI UTEKELEZAJI WA ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI KATIKA MIRADI YA MADARASA YALIYOJENGWA KUTOKANA NA FEDHA ZA UVIKO 19


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Katavi Beda Katani akitoa mchango wake katika Ujenzi unaoendelea kwenye Shule ya Sekondari Kasansa iliyopo kata ya Maji moto Halmashauri ya Mpimbwe

Na Irene Temu

Katavi

Kamati ya siasa ya Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Katavi kupitia Mwenyekiti wake Beda Katani wameupongeza Uongozi wa Serikali ya Mkoa wa Katavi kwa kusimamia kwa umakini na weledi mkubwa miradi ya Ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlele na Halmashauri ya Mpimbwe yaliyojengwa kutokana na fedha za Mapambano dhidi ya Uviko 19 kutoka IMF.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Katavi Beda amesema kitendo Cha Halmashauri ya Mlele kukamilisha Ujenzi wa vyumba vya madarasa na kubakiza ziada ya zaidi ya shilingi Milioni 100,halijawahi kutokea hivyo inaonyesha ni namna gani serikali wamesimamia miradi hiyo kwa uaminifu wa hali ya juu.

Katika pongezi hizo aliendelea kusisitiza swala la amani na mshikamano  baina ya Viongozi kuanzia ngazi za juu hadi kwenye shina lengo likiwa ni kushirikiana katika shughuli za Maendeleo kwani pasipo na maelewano Maendeleo hayawezi kupatikana.

Mwenyekiti Beda aliwataka Wenyeviti wa serikali za Mitaa kuwasomea wananchi taarifa ya mapato na matumizi ili kuondoa maswali juu ya fedha zilivyotumika na kuona kuwa mchango wao katika kuchangia Ujenzi wa miradi inayoendelea katika Halmashauri hiyo unadhaminiwa.

"wananchi wasomewe mapato na matumizi na kuonyesha ule mchango wao walioutoa wakati miradi hii inaendelea kwa kusogeza tofali,kubeba mchanga,kuchota Maji na mengineyo umedhaminiwa"alisema Mwenyekiti Beda

Mjumbe wa kamati ya siasa Mkoa wa Katavi ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko katika ziara iliyoanzia Shule shikizi ya Msingi Utende iliyojengwa vyumba vya madarasa 3, Shule ya Sekondari Inyonga vyumba vya madarasa 3 na Shule ya Sekondari Ilela vyumba vya madarasa 2 katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlele na Shule ya Sekondari Kasansa vyumba 2 pamoja na Shule ya Sekondari Mbede vyumba vya madarasa viwili katika Halmashauri ya Mpimbwe 

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko akimpatia mwanafunzi Peter Christopher fedha kwa ajili ya kununua viatu na Sweta katika Shule shikizi ya Msingi Utende kwenye ziara na Kamati ya siasa Mkoa wa Katavi kukagua mradi wa vyumba vya madarasa yaliyojengwa kwa fedha za Uviko 19 na Shule hiyo ikiwa miongoni mwa Shule iliyojengwa Madarasa matatu.

Aliwataka wanafunzi wa Shule zote kusoma kwa bidii na kuzifikia ndoto zao kwani serikali tayari imekwisha tengeneza miundombinu mizuri ya Elimu kazi ni kwao  kutulia na kusoma.

Pamoja na hayo aliwahimiza wazazi wote ambao watoto wao wamechaguliwa kujiunga kidato cha kwanza katika shule zote zilizopo ndani ya Wilaya ya Mlele na Mpimbwe kuhakikisha  wanakwenda Shule kutoka na idadi ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga katika Shule ya Sekondari  Kasansa na Mbede kutoridhisha.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Teresia Irafay ameeleza kuwa Ujenzi wa vyumba vya madarasa 34 vimekamilika na walipokea jumla ya shilingi Milioni 680 huku wakibakiwa na kiasi Cha zaidi ya shilingi milioni miamoja na fedha hizo wanampango wa kujenga shule ya English medium katika Halmashauri hiyo ya Mlele ikumbukwe fedha hizo ni mkopo kutoka IMF zilizotolewa kwa ajili ya Mapambano dhidi ya Uviko 19.

HABARI PICHA


Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko (kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Mlele Filberto Sanga(katika) na Mratibu wa Ilani ya Cha Chama Mapinduzi Mkoa wa Katavi  Ananias John(kulia) katika ziara ya Utekelezaji wa Ilani ya Cha Chama Mapinduzi 2020/2025 katika Mkoa wa Katavi



Afisa Elimu Mkoa wa Katavi Dr.Baganda Elpidius alisisitiza kwa Waalimu Wakuu wote wa Shule za Sekondari kuwa kwa wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza hakuna kigezo chochote cha kumzuia mwanafunzi kuanza masomo hata akiwa hana sare ya Shule,viatu na vitu vingine anaruhusiwa kuwa darasani na utaratibu mwingine utaendelea akiwa shuleni anasoma.




Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Katavi Beda Katani (katikati) akiteta Jambo na Katibu wa CCM Wilaya ya Mpanda Mwalimu Deus(kushoto) baada ya kukagua shule ya Sekondari Inyonga ambayo ni miongoni mwa Shule zilizojengwa vyumba vya madarasa kwa fedha za Uviko 19.
















 



Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages