VIONGOZI WA DINI NA WAZEE MAARUFU WAFURAHISHWA KUSHIRIKISHWA KUONA MIRADI YA UVIKO 19 MKOA WA KATAVI

 

     

Viongozi wa Madhehebu mbalimbali ya dini,Wazee maarufu pamoja na Viongozi wa  Mkoa wa Katavi wakimsikiliza Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mpanda Haidary Sumry akieleza namna wakazi wa Mkoa wa Katavi watakavyonufaika na ujenzi wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Katavi utakapomalizika.

Na Walter Mguluchuma

 Katavi  

Viongozi wa madhehebu mbalimbali ya Dini,Wazee maarufu na vyama vya siasa Mkoani Katavi wamefurahishwa na hatua ya Serikali ya Mkoa kuwashirikisha kukagua miradi iliyotekelezwa kutokana na fedha za Uviko 19 na miamala ya tozo mbalimbali za mashirika ya simu. 

Kauli hiyo wameitolewa wakati wa ziara waliyoifanya ya kutembelea miradi mbalimbali  ya vyumba vya madarasa,mabweni,vituo vya afya pamoja na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa inayojengwa eneo la Rungwa ziara iliyoandaliwa na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi kwa ajili  ya kuona jinsi fedha za uviko 19 na tozo za miamala ya simu zilivyotumika katika kutekeleza miradi ya maendeleo Mkoa wa Katavi.

Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea miradi hiyo Mwenyekiti wa Wazee Mkoa wa Katavi Thomasi Ngozi ameeleza kuwa ni mara ya kwanza kundi hilo kushirikishwa katika ziara ya kutembelea miradi iliyotekelezwa na inayoendelea kutekelezwa katika Mkoa.

 "haya ni mapinduzi makubwa yaliyofanyika katika kuleta maendeleo kwani tumeweza kujionea wenyewe jinsi ambavyo  miradi ya fedha za uviko 19 na fedha  za miamala ilivyoweza  kutekelezwa kwa ustadi mkubwa katika Mkoa "alisema Mzee Ngozi

Nae Mzee Vicenti Nkana alisema kuwa Rais Samia  Suluhu Hassan amekuwa muwazi kwa kuwaambia wananchi kila Serikali inapokopa fedha kutoka kwa wahisani na malengo ya kukopa fedha hizo tofauti na ilivyokuwa hapo awali .

Mwenyekiti wa Mila na Desturi Mkoa wa Katavi Michael Lusambo hakusita kumwombea Rais Samia asikate tamaa kwa kazi anazozifanya na Mungu azidi kumtia shime  kwa kazi anazoendelea kuzifanya.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Mwanamvua Mrindoko nae alieleza kuwa  Mkoa wa Katavi hadi sasa umeisha pokea zaidi ya shilingi bilioni 33 kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo ni vyumba 425 vya madarasa ambayo yamekamilika kwa asilimia 100, ujenzi wa barabara , Hospitali ya Rufaa  ya Mkoa,Hospitali za Wilaya na vituo  vya afya

 Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Mkoa wa Katavi Joseph  Mona  alieleza kuwa nia ya Rais kuleta fedha Mkoa wa Katavi ni njema  hivyo ni vema watu waliopewa jukumu la kusimamia miradi hiyo wakalifanya kwa uadilifu mkubwa na uaminifu.

 Nae  Meya wa Manispaa ya Mpanda Haidary Sumry amebainisha kuwa miradi hiyo imekuwa ni chachu ya maendeleo  katika Mkoa na imetowa ajiri kubwa kwa vijana wa Mkoa wa Katavi.


Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Katavi Teonas Kinyonto akieleza mbele ya Viongozi wa Dini, Wazee Maarufu na Viongozi wa Mkoa wa Katavi namna Vijana walivyonufaika na fedha za Uviko 19 na tozo za miamala ya simu ambapo ameeleza Vijana wengi wamenufaika kwa kupata ajira kupitia miradi hiyo.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages