ZAIDI YA BILIONI 27 ZAPITISHWA RASIMU YA BAJETI HALMASHAURI YA TANGANYIKA

 

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Tanganyika  Hamad Mapengo akifungua  Kikao cha Baraza la Madiwani wakati wa kupitisha Rasimu ya Bajeti ya Halmashauri hiyo ambapo Baraza limepitisha kwa mwaka 2022/2023 kiasi cha zaidi ya shilingi Bilioni 27


Na  Walter  Mguluchuma

    Tanganyika

Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi limepitisha rasimu ya bajeti ya fedha kwa kipindi cha mwaka 2022/2023 kiasi cha zaidi ya shilingi Bilioni 27 ikiwa ni  ongezeko la asilimia 2.06 ya bajeti ya msimu uliopita .

Akiwasilisha Rasimu ya Bajeti hiyo mbele ya Kikao cha Baraza la Madiwani  Afisa Mipango wa Halmashauri ya Tanganyika  Doto Kwigema alieleza kuwa bajeti hiyo  imezingatia mahitaji muhimu  ya  Halmashauri na wananchi wa ngazi  zote  na mwongozo wa mpango wa bajeti.

Amebainisha kuwa kwa mwaka wa fedha 2022/ 2023 Halmashauri hiyo imepanga kutumia kiasi cha shilingi  27,157,790,000 kati ya fedha hizo  mapato ya ndani ni kiasi  cha shilingi  Bilioni 4,931,335.

Afisa Mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Doto Kwigema akiwasilisha Rasimu ya Bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika  mbele ya Kikao cha Baraza la Madiwani waliopitisha Rasimu hiyo ya bajeti ya zaidi ya shilingi Bilioni 27

 Amesema kuwa  bajeti hiyo imeongezeka  kutoka  Tshs  26,326,111,169 Bajeti ya mwaka 2021/2022 kwa kiasi cha zaidi ya bilioni  27.1 ambayo ni sawa na asilimia 3.06

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Tanganyika Hamad Mapengo  aliwasisitiza Madiwani na Watumishi wa Halmashauri hiyo kuhakikisha wanashirikiana katika kukusanya mapato ili Halmashauri iweze kuwahudumia wananchi wake na kukua zaidi.

Alisema pamoja na kuwa wamepitisha Rasimu hiyo ya Bajeti yeye kama Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo haoni kama itakuwa dhambi kukusanya mapato ya ndani zaidi ya makisio waliyoyaweka.

Diwani wa Viti Maalum Theodela Kisesa alishauri kuwa  fedha ambazo zimepitishwa kwenye Rasimu hiyo ya bajeti za kupambana na afua za Ukimwi bado hazi toshi kwani tatizo hilo bado lipo kwenye Halmashauri hiyo.

 

 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages