AFARIKI KWA KUPIGWA NA RADI CHUMBANI KWAKE

 


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi ACP Ali Makame Hamad


Na Walter Mguluchuma

    Katavi .

 Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la  Lucia  Chaya (15) Mkazi wa  Kijiji cha Tumaini  Kata ya Itenka Wilaya ya Mpanda  amefariki Dunia  hapo hapo  baada ya kupigwa na  radi wakati akiwa chumbani   kwake na mtu mwingine mmoja amejeruhiwa waliyekuwa wakiishi nae kwenye nyumba moja .

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi    All  Makame Hamad amewaambia Waandishi wa habari kuwa tukio hili limetokea hapo  juzi majira ya saa kumi na mbili jioni huko katika Kijiji cha  Tumaini   Kata ya Itenka  Wilaya ya Mapanda .

Kamanda Hamad amesema  marehemu huyo alipigwa na radi na kufariki dunia hapo hapo wakati akiwa amelala chumbani kwake na kumjeruhi mtu mmoja aliyekuwa akiishi naye ndani ya Nyumba hiyo.

Alifafanua kuwa kufuatia mvua  nyingi zinazoendelea kunyesha kwenye maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Katavi  huku zikiwa zimeambatana na upepo mkali ndio chanzo Cha kifo hicho.

"nikwamba  katika tukio hilo mtu mmoja pia  amejeruhiwa  kwa kupigwa na radi  ambae anafahamika kwa jina la  Anna  John(38) Mkazi wa  Kijiji cha  Tumaini  Kata ya Itenka  ambaye walikuwa wamepanga nyumba moja na marehemu huyo lakini wakiishi kwenye vyumba tofauti.

Kamanda  All Hamad amesema kuwa  mara baada ya tukio  hilo Anna  John alikimbizwa  katika zahanati  ya Itenka   kwa ajili ya kupatiwa matibabu  na hali yake kwa sasa inaendelea vizuri.

Katika tukio lingine huko katika  Kitongoji  cha Moto moto Kijiji cha Mapili  Tarafa ya Inyonga Wilaya ya Mlele  mvua kubwa iliyonyesha na kuambatana na radi imepiga nyumba mbili za familia moja  ya Kisinza  Saluhe (93) .

Kamanda Hamad  amesema tukio hilo limetokea juzi majira ya saa  mbili na nusu usiku ambapo katika tukio hili hakuna madhara yoyote kwa binadamu yaliyotokea  isipokuwa  mali  iliyokuwemo  ndani na vyombo  pamoja na nguo  zimeteketea  kwa moto uliosababishwa na radi  hiyo .

Amebainisha kuwa  thamani ya vitu hivyo vilivyoteketea vya kikongwe huyo  vina thamani ya shilingi laki saba na nusu.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages