AMCOS KUIMARISHWA KWA USTAWI WA KILIMO

 

Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne Dr Jakaya Mrisho Kikwete(kulia)


Na  Walter  Mguluchuma

     Katavi

Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho  Kikwete ambae ni Mjumbe wa Bodi ya Shirika la Kimataifala la AGRA linalojishughulisha na kuinua hali ya  kilimo cha wakulima wadogo  ili wazalishe chakula zaidi  na kuangalia usalama wa chakula wa  nchi za  Afrika ikiwemo  Tanzania  ameshauri vyama vya Msingi Amcos kuimarishwa  ili kuweze kusaidia upatikanaji wa masoko ya uhakika  kwa wakulima .

Ushauri huu ameutowa kwa wakati tofauti alipokuwa akiongea na wakulima wadogo wa Wilaya ya Mpanda,Mlele na Tanganyika wakati wa ziara yake katika Mkoa wa Katavi ya kutembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa na Shirika hilo la AGRA.

Amebainisha kuwa hali ya masoko ya wakulima kwa sasa hapa nchini imetetereka  hivyo ni vema   ikaonekana  namna bora ya kujiimarisha vyama vya msingi vya wakulima ili kuweza kusaidia wakulima .

Dkt  Kikwete ameeleza kuwa vyama vya msingi endapo vitaimarishwa  vitasaidia sana kutafuta masoko ya kuuza mazao ya wakulima wao kwenye vyama vyao  kwani Amcos zikiwa imara   hata urahisi wa kupata masoko utakuwepo kuliko ilivyo sasa ambapo Amcos nyingi hazipo imara.

"vyama vingi  vya Ushirika vimekuwa havifanyi vizuri kutokana na aina ya viongozi ambao wamekuwa  wakiviongoza kwani baadhi yao wamekuwa sio waaminifu na nakumbuka wakati wa utawala wangu Serikali ililazimika kulipa kwenye mabenki madeni yote ya vyama vya ushirika hivyi sipendi tena vyama vifikie kwenye hali hiyo"alisema Dkt Kikwete

Amebainisha pia kuna haja ya Wizara ya Kilimo kuangalia namna ya kuweka mpango wa kutowa  ruzuku kwa wakulima kwani kwa sasa  wakulima wengi ndio imekuwa kilio chao ingawa hapo nyuma  serikali iliwahi kutowa ruzuku kwa wakulima kwenye pembejeo  kupitia mawakala  waaminifu hivyo inatakiwa kuwepo  na njia bora zaidi kuliko ya awali.

Dkt  Kikwete amesema kuwa ziara aliyoifanya haina uhusiano na  Urais mstaafu kwani  Tanzania hakuna kazi ya Rais Mstaafu yeye amefanya ziara kama Mjumbe wa bodi ya shirika la Kimataifa la AGRA.

Naibu Waziri wa Kilimo   Antony Mavunde ameeleza kuwa Serikali imerahisisha utaratibu wa utowaji wa vibali vya kusafirishia mazao  nje ya nchi ambapo hata mwananchi wa kijijini anaweza kuomba kibali akiwa kijijini kwake kwani vibali hivyo vinatolewa kwa njia ya mtandao.

 Amesema kuwa katika kuimarisha soko la  kuuzia mazao nje ya nchi serikali imeweka vituo vya kufikishia mazao ya wakulima wanao safirisha mazao yao  nje ya nchi na tayari wanavituo katika nchi za  Sudani ya kusini katika mji wa JUBA  na  Lugumbashi  nchini Congo.

Nae Meneja wa kiwanda cha kusindika mazao ya nafaka cha Flamingo Food Company Ltd kilichoko  Kata ya Majimoto Halmashauri ya Mpimbwe Justine  Mpangala amesema Kampuni ya Flamingo ilifanikiwa kuongeza kipato cha wakulima kwa kununua wastani wa Tani Elfu moja za Mpunga na kutoa Ajira kwa wananchi baada ya kupata Ufadhili kutoka AGRA hivyo kusaidia kuinua uchumi wa nchi na familia pia.

Aidha Mpangala amesema wanamshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha mazingira ya kazi za uwekezaji katika sekta ya Viwanda na Kilimo kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages