AKUTWA NA BANGI CHUMBANI MKOA WA KATAVI

Picha na Mtandao

 Na  Walter Mguluchuma

   Katavi .

 Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi  linamshikilia  Alex Kasambe  Mkazi wa Tambukareli Manispaa ya Mpanda kwa kumakamata na dawa za kulevya aina ya bangi debe mbili akiwa ameficha ndani ya chumba chake anachoishi .

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi All Makame  Hamad amewaambia Waandishi wa Habari mtuhumiwa huyo alikamatwa Machi 12 majira ya saa sita usiku huko katika Mtaa wa Tambukareli alikokuwa akiishi .

Alisema mtuhumiwa alikamatwa kufutia Jeshi hilo la Polisi kupata taarifa za mtumiwa huyo kuwa ana jihusisha na biashara ya kuuza dawa za kulevya aina ya bangi .

Baada ya Jeshi hilo kupata taarifa lilianza kufanya uchunguzi  na ndipo baada ya kukamilisha uchunguzi walifanikiwa kumkamata  mtuhumiwa  Alex Kasambe akiwa na debe mbili za bangi .

Kamanda All  Makame  Hamad  ameeleza kuwa  mtuhumiwa huyo alikamatwa  akiwa amehifadhi bangi hiyo debe mbili katika mfuko  wa sandarusi  huku akiwa ameificha kwenye chumba chake cha kuishi .

Mtuhumiwa  bado anashikiliwa na Jeshi la Polisi  kwa mahojiano zaidi  kwa lengo  la kupata  mtandao mzima  wa  kuwapata watuhumiwa wengine ambao wamekuwa wakijihusisha na biashara hiyo haramu.

Upelelezi utakapo kamilika mtuhumiwa Alex Kasembe  atafikishwa mahakamani  ili kujibu tuhuma  inayomkabili ya kupatikana na debe mbili za dawa za kulevya aina ya bangi .

Aidha  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi amewapongeza wananchi  wanaojitowa kushirikiana  na Jeshi la Polisi kwa kuwapatia taarifa za uhalifu  zinazosaidia  kuuweka Mkoa wa Katavi  kuendelea kuwa salama.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages