AMUUWA MKE WAKE NA MTOTO KISHA KUWAFUKIA ARDHINI

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi ACP Ali Makame Hamad


Na Walter MguIuchuma

  Katavi

Watu wawili  wakazi wa  Vijiji vya  Nkungwi na Sentamaria Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi wanashikiliwa na Jeshi la Polisi akiwemo  mume wa marehemu  Dutu Maige  na Yusuph Sita  kwa tuhuma za  kumuuwa Mariamu Paschal(36) na mtoto wake  Editha Dutu(04)  kisha kuwafukia  kwenye shimo kufuatia  ugomvi wa kugombania gunia sitini za mpunga .

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi  All Makame  Hamad watuhumiwa hao  wamekamatwa  Machi9,2022 kufuatia Upelelezi uliofanywa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi 

Amebainisha kuwa Jeshi hilo  lilipokea  taarifa kutoka kwa  Paschal Masheku  mkazi wa kijiji cha Sentamaria  ambae ni Baba mzazi wa Marehemu  Mariamu  kuwa  mtoto wake aitwaye Mariamu Paschal na  Mjukuu wake Editha  Dutu  wametoweka katika mazingira ya kutatanisha tangu  Julai  2021 .

 Baada ya Jeshi la Polisi  kupokea  taarifa hizo  Upelelezi wa kina ulianza mara moja  na ndipo tarehe 9 March watuhumiwa hao  wawili ambao ni Dutu  Maige na  Yusup  Sita  walikamatwa kuhusiana na mauaji hayo .

Kamanda All Makame   Hamad  ameeleza kuwa  baada ya watuhumiwa hao kukamatwa na  kufanyiwa mahojiano wote wawili  kwa pamoja  walikiri  kumuuwa  Mariamu  Paschal na mtoto wake  Editha  Dutu  na kisha miili yao kuifukia katika shimo  kwenye pori la Kalilankulunkulu  lililopo kwenye mashamba ya Magereza  Wilaya ya Tanganyika.

Baada ya kukiri kutenda mauaji hayo ndipo March 12 mwaka huu watuhumiwa hao wote wawili  waliwaongoza  Askari wa Jeshi la Polisi  kuonyesha  mahali ilipo miili  hiyo ya marehemu hao .

Baada  ya kufukua kwenye shimo hilo  yalipatikana mabaki ya miili ya marehemu hao ya sehemu ya mbavu na kichwa .

Kamanda Hamad ameeleza kuwa  chanzo cha tukio hilo ni ugomvi wa kifamilia  kati ya mtuhumiwa  Dutu  Maige  na aliyekuwa mkewe Mariamu Paschal waliokuwa wakidaiana gunia sitini za mpunga .

Upelelezi  wa  tukio  hili bado unaendelea   na mara  utakapokamilika watuhumiwa hao wote  watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazo wakabili .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages