MHABESHI AKAMATWA AKIWA SAFARINI MKOA WA KATAVI BILA KIBALI


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi ACP Ali Makame Hamad


Na Walter  Mguluchuma

Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi limemkamata  Mamshi  Abagashi Seleko(33) Raia wa Nchi ya Ethiopia  akiwa ameingia nchini bila kibali kwa kutumia gari akielekea katika Mji wa Mpanda .

Kamanda wa Polisi wa  Mkoa wa Katavi Ali  Makame Hamad amewaambia Waandishi wa Habari  kuwa  raia huyo wa kigeni alikamatwa na Jeshi la polisi  Mkoa wa Katavi  wakati lilipokuwa likifanya msako kwenye maeneo mbalimbali ya Mkoa huo.

Alisema  mtuhumiwa huyo alikamatwa katika kijiji cha  Mirumba Tarafa ya  Mpimbwe Wilaya ya  Mlele Mkoa wa Katavi akiwasafarini akitumia gari  lenye namba za usajiri  T.743 DMA aina ya Toyota  Land cruiser V-8 VX mali ya  Mwaipopo  Mark Mkazi wa Dares salaam.

Kamanda Hamad  alieleza  baada ya  tukio hilo dereva  wa gari hilo alitoroka na kutokomea kusiko julikana na kumwacha raia huyo wa kigeni akiwa mikononi mwa Jeshi la Polisi .

Juhudi za kumsaka  dereva huyo na Mmiliki wa gari hilo  zinaendelea kwa ushirikiano wa Jeshi la Polisi na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)  na Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Katavi.

Mtuhumiwa huyo  baada ya kuhojiwa na Jeshi la Polisi  amekabidhiwa Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Katavi  kwa hatua  zaidi za kisheria.

Katika tukio jingine  Kamanda Ali Makame Hamad amesema  watu wawili waliofahamika kwa jina la  Faines  Mihani(37) na Elizabet Nyandwi (13) mwanafunzi  wa darasa la sita Shule ya Msingi Mlibanzi    wamefariki dunia  hapo hapo  baada ya kupigwa  na radi  wakati wakiwa shambani wanalima.

Amesema tukio hilo limetokea katika kijiji  cha Mlibanzi  Kata ya Ipwaga   Mishamo Tarafa ya Kabungu Wilaya ya Tanganyika.


 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages