MKOA WA KATAVI KUTOKOMEZA UGONJWA WA TB KWA JAMII KUJITOKEZA KUPIMA


Mratibu wa Kudhibiti Ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB) na Ukoma Manispaa ya Mpanda Bruno Cronely leo March 24,2022 katika maadhimisho ya kilele Cha Ugonjwa huo yaliyofanyika katika mtaa wa Mnazi Mmoja kata ya Uwanja wa Ndege na  Nsemulwa Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi


 Irene Temu

Katavi

Wananchi wa Mkoa wa Katavi wamekuwa na  dhana potofu juu ya  Ugonjwa wa Kifua Kikuu wakiamini ugonjwa huo unatokana na  kulongwa  hali ambayo imekuwa ikisababisha kushindwa kupatiwa matibabu kwa wakati kabla ya Ugonjwa haujakomaa

Hayo yameelezwa na  Mratibu  wa Kudhibiti Ugonjwa  Kifua Kikuu na  Ukoma Manispaa ya Mpanda   Bruno  Cronely wakati  wa mafunzo ya kuwajengea uwezo Waandishi wa Habari wa vyombo mbambali wa Mkoa wa Katavi  Juu ya Kuandikia,Kutangaza  na kuripoti maswala ya ugonjwa wa TB yaliofanyika kwenye Ukumbi wa Kichangani katika Manispaa ya Mpanda .

Amebainisha kuwa  baadhi ya wananchi kukosa uelewa juu ya Ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB)imekuwa sababu ya wanaougua ugonjwa huo  kuamini wamelogwa kitu ambacho  sio sahihi katika afya ya binadamu .

Alisema kuwa Ugonjwa wa  Kifua Kikuu hauenezwi kwa njia  za kishirikina bali  ni ugonjwa unaoenezwa kwa  njia ya hewa  ambayo hupelekea  mgonjwa  wa ugonjwa huu kukohoa kikohozi  kikali na kikavu  kwa muda wa wiki mbili na kuendelea.

Cronel  amesema kuwa mafunzo hayo waliopatiwa Waandishi wa Habari  yatasaidia kuwa mabalozi wazuri  kwa kuelimisha kwa ufasaha Jamii kuhusu Ugonjwa wa  Kifua Kikuu.

Amefafanua kuwa  Manispaa ya Mpanda  kwa mwaka 2019 walipanga kuwaibua  wagonjwa 340 hata hivyo wameweza kuvuka lengo na kuwaibua wagonjwa  435 ambao ni  sawa na asilimia  127.

Kati ya wagonjwa hao  idadi ya waliofariki dunia ni wagonjwa  23 hali inayoonyesha kuwa ugonjwa huo sio wa kupuuzia hata kidogo kwani umekuwa ukisababisha vifo vya watu katika Jamii.

Kwa hapa nchini  mwaka huo wa  2019 Jumla ya watu 137,000  waliugua ugonjwa wa TB  ambao kati yao watu 81,000 walianzishiwa Matibabu ya Dawa sawa na asilimia  59 ambao kati ya watu hao  watu 74,000 walitibiwa na kupona kabisa.

Amewataja  waathirika wakubwa wa ugonjwa wa Kifua Kikuu ni makundi ya wazeee, watoto na waathirika  wa Ugonjwa  wa  Ukimwi  na ameitaka jamii kuwa na utamaduni  wa kufika kwenye vituo vya afya  vya serikali  kwa ajili ya kufanyiwa vipimo pindi wanapokuwa wamehisi dalili za  kuwa na Ugonjwa  Kifua Kikuu.

Kwa upande wake  Mwezeshaji wa  huduma za Jamii  kutoka Amref  Keneth Simbaya  alisema wamechagua  kundi la Waandishi wa Habari  kuwapatia elimu hiyo ya Ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB)kwa kuwa wana nafasi kubwa kupitia vyombo vyao vya habari kuifikia Jamii.

"...... naamini jamii ya watu wengi haifikiwi  vya kutosha  na kufahamu zaidi  kuhusu ugonjwa wa kifua kikuu hivyo kwa kupitia  mafunzo haya tuliyowapatia Waandishi wa Habari  wataisaidia serikali  katika mpango  wake wa kukomesha  Ugonjwa wa Kifua Kikuu hapa nchini ifikapo mwaka 2030.

Simbaya amesisitiza kuwa wao kama  Amref wanatowa  Maudhui  kwa Waandishi  wa Habari  ili wafanye kazi kwenye jamii  kwa kujikita  katika utatuzi  wa tatizo la ugonjwa huo kwa  kushirikisha wataalamu  wabobevu  katika eneo hilo.

Mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo  Mwandishi wa Habari  Uhuru Media  Irene  Temu  alisema kuwa jamii  nyingi zimekumbwa na ugonjwa huo kwa kutojua chanzo  na matibabu  hivyo mafunzo aliyoyapata yataikomboa jamii kwa kuwapa Elimu kupitia chombo chake Cha Habari.

Zilipa Joseph Mwandishi wa ITV Mkoa wa Katavi  kupitia mafunzo hayo amepongeza na kusema yamekuja kwa wakati  sahihi  kutokana na baadhi ya jamii kuwa na dhana potofu  kuhusiana na Ugonjwa wa Kifua Kikuu na ameahidi Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Katavi watajikita kuelimisha jamii kupitia vyombo vyao mbalimbali vya habari .

 

 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages