MUME AMCHINJA MKE WAKE NAE AJINYONGA

 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi ACP Ali Makame Hamad akitoa Taarifa ya Matukio mbalimbali yaliyotokea ndani ya Mkoa wa Katavi mbele ya Waandishi wa Habari leo Mach 4,2022


Na  Walter  Mguluchuma

    Katavi

 Mtu mmoja aliyefahamika kwa  jina la Jeniviva Timotheo(29)  Mkazi wa Kijiji cha Mtakuja Kata ya Nsekwa Tarafa ya Inyonga Wilaya ya Mlele  Mkoa wa Katavi ameuawa kikatili  kwa kuchinjwa na panga shingoni na mume wake aitwaye  Anisent John(32) na baada na kumchinja nae akajinyonga juu ya dari na kuacha ujumbe wa maandishi .

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi ACP Ali Makame Hamad amewaambia Waandishi wa Habari kuwa mauwaji  hayo ya kikatili  na yakusikitisha  ya  mwanamke  huyo  yametokea Machi 2 majira ya saa tisa mchana huko nyumbani kwa wanandoa hao wawili waliokuwa wakiishi katika kijiji cha Mtakuja .

Alisema  mtuhumiwa wa mauwaji hayo ambae ni  marehemu  kabla ya kutekeleza mauwaji hayo alivizia watoto wao wakiwa shuleni ndipo alipotekeleza mauaji hayo.

Ni kwamba kabla ya kufanya mauwaji hayo mtuhumiwa ambaye pia ni marehemu alifunga milango yote ya nyumba yake na kubaki ndani yeye na mke na ndipo alipomuuwa kikatili Mkewe huyo kwa kumchinja na panga shingoni pasipo watu kujua.

Kamanda All Makame Hamad ameeleza kuwa baada  ya kutekeleza mauwaji hayo mtuhumiwa  nae aliamua kujinyonga  kwa kutumia  chandarua  kwa kujining'iniza kwenye  kenchi  ya dari ndani ya chumba alichofanyia mauwaji ya mke wake.

Amesema kuwa  taarifa za vifo vya wanandoa hao viligundulika baada ya mtoto wao mmoja aliyekuwa ametoka shuleni  kufika nyumbani na kukuta milango yote ya nyumba imefungwa licha ya kufanya jitihada za kufungua alishindwa na kulazimika kwenda kutoa taarifa kwa mjomba wake aliyekuwa akiishi jirani na walipofika eneo la tukio walivunja mlango na kukuta ndani miili ya Marehemu hao .

Majirani walifika nyumbani kwa marehemu hao baada ya kusikia kilio cha mtoto wa marehemu na kisha kutowa taarifa Kituo cha Polisi  ambao walifika eneo hilo na walipoingia ndani kwenye chumba cha marehemu hao  na walikuta ujumbe wa maandishi  uliokuwa umeandikwa  na Marehemu  Anisent John usemao amejiuwa kwa hiari yake mwenyewe.

Kamanda Hamad amesema chanzo  cha tukio hilo ni mgogoro baina yao wakifamilia unaohusishwa  na wivu  wa kimapenzi  ambapo mke alikuwa akimtuhumu mumewe kuwa  na wanawake wengine kijijini hapo .

  

 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages