ASOMBWA NA MAJI AKIVUKA MTO

Picha na Mtandao

Frida Gonzi,Mpanda

MKAZI wa kijiji cha Kakese tarafa ya Misukumilo Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi anayefahamika kwa jina moja Mungo amesombwa na maji wakati akivuka mto kwenda mnadani huku akiwa amebaba zaidi ya fedha mil moja na laki tano.

Imetajwa kuwa chanzo cha kusombwa na maji ni ubovu wa miundombinu ya barabara hususani ya kukosekana kwa madaraja na makalvati imari imara yatakayowasaidia wananchi kuvuka kwa usalama zaidi.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mbugani Kata ya Kakese, Boniface Sendelali amesema kuwa mtu huyo amesombwa na maji  hapo juzi majira ya saa mbili asubuhi kwenye eneo la mto unaounganisha vijiji vya Kakese na Kijiji cha Itenka.

Amesema siku hiyo ya tukio  mtu huyo aliaga familia yake kuwa anakwenda kwenye mnada wa ng'ombe katika Kijiji jirani cha Itenka kwa lengo la kwenda kununua  ng'ombe na aliondoka akiwa amebeba kiasi cha Tshs 6,680,000.

Amebainisha kuwa kwenye msafara huo alikuwa ameambatana na wanakijiji wenzake ambao nao walikuwa wakielekea kwenye mnada huo kwa lengo la kwenda kununua Mifugo.

Baada ya kuwa wameanza safari yao  kuelekea Kijiji cha Itenka walifika kwenye mto ambao unaunganisha vijiji hivyo viwili na walikuta mto umejaa na maji yakiwa yanapita kwa kasi kwenye mto huo.

Nao baadhi ya wananchi wa kijiji cha Kakese,Mariam Rashid amesema kuwa serikali inapaswa kufanyia kazi kero ya ubovu wa miundombinu ya barabara kwani kwa muda mrefu sasa inawapa wakati mgumu kuvuka katika mto huo.

“Kifo hiki kimetusikitisha sana.Sisi tukiwa wanawake ndio wahanga wakubwa wa ubovu wa barabara na ubovu wa madaraja ambapo tunashindwa kuvuka wakati tukiwa kwenye majukumu yetu ya kila siku hususani ya kwenda kuteka maji” Amesema Mariam.

Janeth Anthony ametoa wito kwa serikali kuimarisha miundombinu ya barabara kwa sababu barabara ni nyenzo muhimu sana kwenye kusafirisha bidhaa hasa za mazao ya kilimo kwani jamii yao niya wakuluma.

“Diwani anapaswa kutambua tumemchangua sio kwa sababu ya kuboresha maisha yake.Haiwezekani vifo vitokee kwa sababu ya ubovu wa daraja” Amesema

Diwani wa Kata ya Kakese,Maganga Salaganda amesema taarifa za kusombwa na maji kwenye mto huo zilifika kwa viongozi wa Kata ambao nao walifanya juhudi za kuanza kumtafuta  kwa mchana na usiku.

Amesema hadi sasa licha ya juhudi hizo kuendelea  mtu huyo  bado haja patikana  na wameamua pia kushirikisha jeshi la jadi la sungusungu  ambao hadi  sasa wapo kwenye eneo hilo la mto wakiendelea kumtafuta.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages