WASIOREJESHA MIKOPO KUSAKWA MANISPAA YA MPANDA

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mpanda Mh. Haidary Sumry

Na Walter MguIuchuma,Mpanda 

Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa  ya  Mpanda  Mkoani   Katavi limeviomba vya usalama  na ulinzi  viwasaidie kuwakamata  wadaiwa sungu waliochukua mikopo ya  makundi maalumu ya vijana ,wanawake na watu wenye ulemavu ambapo hadi sasa asilimia  arobaini ya mikopo iliyotolewa na Manispaa ya Mpanda  haija  rejeshwa .

 Azimio hilo la Baraza la Madiwani  lilipitishwa  kwenye kikao hicho kufuatia taarifa  ya kutoridhisha ya urejeshaji wa mikopo hiyo kwa makundi hayo kwa kipindi cha mwaka huu wa fedha 2021/2022.

Meya wa Manispaa ya Mpanda  Haidary Sumry alieleza kuwa hadi sasa ni asilimia 53 tuu ya fedha za mkopo wa makundi maalumu ya  vijana,wanawake na watu wenye ulemavu ambazo zimerejeshwa kwa vikundi ambavyo vilipatiwa mikopo huku ikiwa asilimia 43  hawaja rejesha mikopo hiyo .

Alisema  wametoa  maelekezo  kwa Mwanasheria wa Halmashauri ya Manispaa kuangalia vikundi vyote ambavyo havija rejesha mikopo hiyo kwani mikataba yao ya mikopo ipo wazi .

Sumry alisema kuwa kama hawata wachukulia hatua watu hao  itaonekana na kwa watu wengine  zinatolewa kama ni sadaka jambo ambolo sio kusudio la kutolewa kwa mikopo hiyo ambayo haina tiba.

Hivyo wameviomba vyombo vya Ulinzi na Usalama  visaidie  kuwakamata watu wote ambao hadi sasa hawajarejesha mikopo hiyo licha ya kuwa wamekuwa wakikumbushwa mara kwa mara lakini wamekuwa hawatekelezi.

 Kaimu  Mkuu wa Takukuru Wilaya ya Mpanda  Ahmed Bukuku  alisema kuwa wako tayari kushirikiana na Manispaa hiyo kuwasaka watu wote ambao hawaja rejesha fedha hizo za mikopo za makundi maalumu .

Alisisitiza kuwa kinachotakiwa Takukuru wapewe orodha ya majina hayo ili zoezi hilo  la kuwasaka lianze mara moja kwani hiyo itakuwa sio mara yao ya kwanza kufanya kazi kama hiyo ya kuwakata wadaiwa sugu wa fedha za mikopo.

 Katika hatua nyingine baraza hilo limempongeza  Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda  Sophia  Kumbuli   kwa kuendesha operesheni  ya kukamata  watoto wanaozurura mitaani muda wa masomo  na kuwachukulia hatua wazazi  wa watoto hao  na Baraza  limeelekeza  zoezi hilo  liwe endelevu.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages