11 MBARONI KWA KUKAMATWA NA VITU VYA WIZI


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi ACP Ali Makame Hamad

Na Walter Mguluchuma .

   Katavi.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi linawashikilia watu kumi  na moja wakiwa na vitu mbalimbali vya  wizi vilivyo ibiwa  kwenye nyumba za watu  zikiwemo TV,Magodoro Mafuta ya Diseli na Pikipiki iliyoibiwa Mkoani Kigoma .

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Ali Makame  Hamad amesema watuhumiwa hao wamekamatwa  kufutia msoko mkali uliofanywa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na wananchi waliotoa ushirikiano kwa Jeshi la polisi .

 Alisema mnamo Aprili 29,2022 Jeshi la Polisi lilimkamata mtuhumiwa  Hadija Ibrahimu (24) Mkazi wa Mtaa wa Nsemlwa akiwa na TV  moja aina ya  Singsung  Flatscreen nchi 21 mali inayodhani kuwa ni ya wizi pia alikamatwa  Christina  Yahaya (41)  mkazi wa Mtaa wa Mnazi mmoja akiwa na godoro moja  5 kwa 6 mali inayodhani kuwa ya wizi .

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi Ali Makame  Hamad akionyesha  mbele ya Waandishi wa Habari baadhi ya vitu walivyokamata kwa watuhumiwa 11 kufuatia  msako uliofanywa na Jeshi hilo na miongoni mwa vitu hivyo ni pikipiki moja iliyoibiwa Mkoani Kigoma,TV, Magodoro,Friji ,Radio pamoja na Mafuta ya dizeli lita 200(Picha na Walter MguIuchuma)


Aidhaalikamatwa mtuhumiwa  Ramadhani Idd akiwa na godoro moja  5 kwa 6,radio moja   aina ya  Sipiano  na speker  zake mbili  vilevile  alikamatwa mtuhumiwa Daud  mkazi wa Mtaa wa Nsemlwa  akiwa na begi  mbili za nguo  ,zulia moja na vyombo mbalimbali  vya ndani .


Kamanda  Ali  Makame Hamad alieleza kuwa kwenye msako huu wamefanikiwa pia kumkamata mtuhumiwa  Joseph   Makame (30) Mkazi wa Mtaa wa Makanyagio akiwa na pikipiki  aina  ya Kinglion yenye Namba za usajiri  MC.755 DCL  ambayo  iliibiwa Mkoani Kigoma .

 Pia  katika msako huo  wamefanikiwa kukamata  Tv moja  aina ya LG  inchi 32,tv  moja aina ya Home  base nchi 50,magodoro matatu,friji moja,radio tatu pamoja na subwoofa aina ya aborder.

Alisema  watuhumiwa hao 11 waliokamatwa bado wanaendelea kushikiliwa na jeshi la polisi  pamoja na walioshirikiana nao kufanya uhalifu wa kuvunja  na kuiba vitu hivyo  ili kuweza kupata  mtandao wote  na mara uchunguzi utakapo kamilika watuhumiwa watafikishwa Mahakamani.

Katika tukio jingine huko katika Kijiji cha Ilalangulu  Kata ya Kibaoni  Wilaya ya Mlele Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi  limewakamata watuhumiwa wanne  wakiwa na mafuta ya dizeli  lita 200 yakiwa yamehifadhiwa kwenye madumu  ya lita ishirini.

Mafuta hayo wameyaiba kwenye Kampuni ya Ujenzi  Morden  Agro Ltd inayofanya kazi ya ujenzi  wa barabara kutoka Kibaoni kwenda Sitalike ambao watuhumiwa hao ni wafanyakazi wa kampuni hiyo.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages