POLISI KATAVI WAIMARISHA ULINZI SIKU KUU YA Eid el Fitri


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi ACP Ali Makame Hamad


 Na Walter MguIuchuma

     Katavi

Jeshi la Polisi  Mkoa wa Katavi  katika kuhakikisha  sikuuu ya Eid  el Fitri inasherekewa kwa amani katika Mkoa huo limejipanga kuimarisha ulinzi  kwenye maeneo yote   na kwenye maeneo ya nyumba  za Ibada pamoja na barabara zinazoingia na kutoka nje ya Mkoa wa Katavi .

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Ali Makame  Hamad amewaambia Waandishi wa Habari  kuwa kama ambavyo watu wanafahamu kuwa waumini wa dini ya Kiislamu  wapo katika  mfungo  wa Mwezi  Mtukufu  wa Ramadhani .

 Hivyo  katika  kuisherekea sikukuu hiyo  kutafanyika ibada kwenye maeneo mbambali ya Mkoa wa Katavi  na moja ya jukumu la Jeshi la Polisi ni kuhakikisha waumini wanafanya ibada kwa amani na utulivu mkubwa .

Kamanda  Ali Makame  Hamad  alisema katika kuhakikisha  sikukuu  hiyo inasherekewa kwa amani  na  utulivu  Jeshi la Polisi  mkoani hapo limejipanga  vyema  kuimarisha ulinzi  kwenye maeneo yote hususani  nyumba za Ibada .

 Amebainisha kuwa kutakuwa na doria  za muda wote  ambapo Askari watakuwa  katika doria  za miguu ,pikipiki pamoja na magari  kwenye maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Katavi.

Amewashukuru wananchi wa Mkoa wa  Katavi kwa ushirikiano wanaendelea kuutoa kwa Jeshi la polisi  kwa kutowa taarifa mbalimbali za uhalifu na  kuweza kusaidia wahalifu kukamatwa kabla ya kufanya uhalifu au baada ya kufanya matukio .

Alisema hali hiyo ya Ushirikiano baina ya Polisi na Wananchi  imepelekea  Mkoa wa Katavi kuwa shwari  kipindi  chote  cha  mwaka huu kuanzia  Mwezi Januari hadi sasa.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages