WANNE WAKAMATWA NA KILO 600 ZA NYAMA YA KIBOKO NA BUNDUKI YA HALMASHAURI YA NSIMBO .

Kaimu Kamanda wa Polisi  Mkoa wa Katavi  Sylivester Ibrahim


 Na  Walter  Mguluchuma

        Katavi .

Watu wanne  wanashikiliwa  na Polisi Mkoa wa Katavi  kwa tuhuma za kuwakamata na kilo 600 za  nyama ya kiboko huku wakiwa na bunduki  aina ya  Rifle  inayomilikiwa na Halmashauri  ya Nsimbo .

Kaimu  Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi amewataja watuhumiwa hao waliokamatwa na nyama ya kiboko kuwa ni Gilberti  Kaswiza (45) Mkazi wa  Ilembo Manispaa ya Mpanda ambae alikuwa na wenzake Wenseslaus  Wiliam (KARUMENDO)ambaye ni Askari  wa  Idara ya wanyamapori Halmashauri ya  Nsimbo,Ally  Juma(41),Mashaka Khamisi (40) pamoja na Kasala  Issa(42) wote wakazi wa Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi.

Alisema watuhumiwa hao walikamatwa Mei8,2022 majira ya saa tisa na nusu mchana  katika Kijiji cha Tulieni Kata ya Itenka  Wilaya ya Mpanda wakiwa wamepakia nyama hiyo ya kiboko kilo 600 kwenye gari  yenye Namba za usajiri T 905 BTM inayomilikiwa  na Joseph Misasi  Fundi magari mkazi wa  Mtaa wa Nyerere Manispaa ya Mpanda .

Watuhumiwa hao  walimuuwa kiboko huyo kwa kutumia silaha  aina ya Rifle  yenye Namba za  usajiri  G.4687  ambayo inamilikiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo .

Amebainisha kuwa kukamatwa kwa watuhumiwa hao kulifuatia  taarifa zilizofikishwa Hifadhi ya Taifa ya Katavi ya kuuwawa kwa mnyama huyo na ndipo walipoanza msako na kuwakamata watuhumiwa hao wakiwa na nyama hiyo.

Watuhumiwa hao wanatarajiwa kufikishwa Mahakamani kujibu tuhuma zinazo wakabili juu ya tukio hilo la kukutwa na nyara za serikali.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages