MBARONI KWA KUM'BAKA NA KUMLAWITI MTOTO WA MIAKA MINNE

 



Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi ACP Ali Makame Hamad akifafanua mbele ya Waandishi wa Habari tukio la mtoto wa miaka minne kulawitiwa.                                        

NA Walter Mguluchuma,Katavi.

JESHI la  Polisi  Mkoa wa Katavi  linamshikilia  Juma Jackson (30) Mkazi wa  Kijiji cha Kagunga Tarafa ya Mwese Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi kwa tuhuma za kumlawiti  na kumbaka  mtoto wa miaka minne  baada ya kuahidiwa  kulipwa ng'ombe watatu baada ya kutenda tukio hilo ili  awatumie kwa ajili ya ushirikina  wa kulinda shamba .

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Ali Hamad  Makame amewaambia Waandishi wa Habari kuwa tukio hilo la kinyama limetokea hivi karibuni katika Kijiji cha Kagunga Wilayani Tanganyika .

Mtuhumiwa  Jackson  siku hiyo ya tukio  alimvizia mtoto huyo jina limehifadhiwa  wakati akitoka  nyumbani kwao kwenda nyumba ya jirani kwa lengo la  kucheza na watoto wenzake.

Amesema Kamanda ndipo mtuhumiwa  alipomkamata  na kumvutia kichakani  kisha alimvua nguo  zake alizokuwa amevaa na kuanza kumbaka na kumlawiti  huku akiwa amemkaba shingoni  na kumwamuru  mtoto huyo asipige kelele za kuomba msaada 

Kamanda  Ali Makame alisema baada ya mtuhumiwa kukamatwa  na Jeshi la Polisi  uchunguzi wa awali  umebaini  kuwa  tukio hilo  linahusiana  na imani za kishirikina  kwani mtuhumiwa  alikuwa amehaidiwa  kulipwa ng'ombe  watatu  baada ya kutekeleza kitendo hicho. 

Alieleza kuwa  mtuhumiwa baada ya kutenda kitendo hicho  alitakiwa  na mtu huyo aliyemtuma  kutekeleza tukio hilo  aende akamwonyeshe  shambani kwake  ili iwe  zindiko  kwa ajili ya shamba  lake lisiwe linaibiwa mazao .

Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi   linaiasa jamii na kukemea vikali  matukio ya namna hii na halita sita  kumchukulia hatua mtu yeyote  atakaebainika  kujihusisha na matendo ya namna hiyo.

Kamanda Makame amesema Jeshi la polisi wanaendelea na  upelelezi  wa tukio hili  na pindi upelelezi utakapo kamilika  mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani mara moja.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages