MKUU WA MKOA WA KATAVI AWAONYA BODA BODA NA WAENDESHA BAJAJI KUTOTUMIKA KWENYE UHALIFU .

Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Mwanamvua Mrindoko  akikabidhi  mmoja wa wanufaika wa mkopo  wa Pikipiki na Bajaji uliotolewa na Benki  ya NMB  kwa ajili ya waendesha Boda boda na Bajaji Mkoa wa Katavi ambapo  NMB wametowa mkopo huo wa zaidi ya shilingi milioni 81.(Picha na Walter  Mguluchuma)


Na  Walter Mguluchuma.

   Katavi .

Mkuu wa  Mkoa wa Katavi Mwanamvua  Mrindoko amewataka  waendesha piki piki(BODA BODA) na waendesha Bajaji kutotumiwa kushiriki  kwenye matukio ya kufanya vitendo  vya uhalifu  kwa kuwabeba wahalifu kwenye vyombo vyao vya usafiri au kuwakodishia watu wanaofanya uhalifu.

 Mwanamvua ametowa maagizo hayo wakati alipokuwa akikabidhi Bajaji  nane na piki piki tatu  zenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 81 zilizotolewa mkopo kwa waendesha boda boda na waendesha bajaji ikiwa ni mkopo uliotolewa na Benki ya NMB  wenye kulenga kupunguza tatizo la vijana wasio na ajira ili waweze kujikomboa kiuchumi.

Alisema kuna tabia  ya baadhi ya boda boda na waendesha bajaji vyombo vyao kutumika kwenye matukio ya uhalifu kwa kuwabeba wahalifu au kuwakodishia usafiri wa vyombo vyao .

Hivyo aliwasisitiza watumie vyombo vyao vizuri kwa ajili ya lengo lililokusudiwa  la kufanyia shughuli za kufanyia usafirishaji  na wafanye shughuli hiyo kwenye maeneo yote ya Mji wa Mpanda  bila kuwakodishia watu kufanyia uhalifu .

Alisema  NMB  wamefanya kazi kubwa ya kutowa mikopo hiyo na inaonyesha jinsi ambayo inaiunga mkono  Serikali kwenye kupunguza tatizo la watu wasio  na ajira hapa nchini  kwani Serikali imekuwa ikisisitiza kila mtu kufanya kazi .

".....hakikisheni vyombo hivyo mlivyokopeshwa mnavitumia kwa kuzingatia  sheria za usalama bara barani vinginevyo  kama hamtotii na kuzingatia sheria za usalama barabarani mtakuwa  mnatishia amani"alisema Mrindoko

Amewata pia waendesha boda boda kufanya kazi kwa bidii ili mkopo huu waliokopeshwa na NMB waweze kuurudisha kwa wakati na hata hapo baadaye kununua vyombo vikubwa zaidi ya hivyo kwani  Mkoa wa Katavi bado una mahitaji ya vyombo vya usafiri 

Baadhi ya wadau waliohudhuria hafla ya kuwakabidhi Dereva Boda Boda na Bajaji mkopo wa Pikipiki na Bajaji uliotolewa na Benki ya NMB tawi la Mpanda Mkoa wa Katavi.(Picha na Walter MguIuchuma)

 Meneja  mauzo wa NMB  Kanda ya Magharibi  Trifon  Melkiory  alisema benki hiyo inaendelea kushirikiana na waendesha boda boda   kwa kuwapatia mikopo kwa kupitia mpango  wa  MASTABODA .

 Alisema kuwa hadi  sasa Mkoa wa Katavi umekuwa na mwitikio mkubwa katika mpango huu na unaongoza kwa kupatiwa  mkopo huu ukifatiwa na Mkoa wa Tabora ambao hadi sasa wamekopeshwa bajaji sita wakati Mkoa wa Katavi wamekopeshwa bajaji nane  na pikipiki tatu .

Mlezi wa Boda boda na Waendesha Bajaji wa Mkoa wa Katavi Beda Katani alieleza kuwa mkopo huo waliopatiwa wasidhani kuwa ni wabure wahakikishe wanarejesha NMB   mkopo huu kwa mujibu wa mkataba wao na benki hiyo ili na wengine waweze kunufaika na mkopo  .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages