NMB YATOWA MKOPO WA BAJAJI NA PIKIPIKI WA ZAIDI YA MILIONI 81 KWA BODA NA MADEREVA WA BAJAJI MKOANI KATAVI

 

Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Mwanamvua Mrindoko  akijaribu kuendesha moja ya bajaji iliyotolewa na  Benki ya NMB  kwa ajili ya waendesha  Boda boda na Bajaji wa Mkoa wa Katavi ambapo NMB wametowa mkopo wa bajaji nane na pikipiki tatu zenye jumla ya zaidi ya shilingi Milioni 81.(Picha na Walter Mguluchuma)


Na  Walter Mguluchuma

     Katavi .

Benki ya MNB imetoa mkopo  kwa waendesha Bajaji na Boda boda wa Mkoa wa Katavi  wenye thamani ya zaidi ya shilingi  Milioni 81 ikiwa ni jitihada za kuiunga Mkono Serikali  kupunguza tatizo la ajira kwa vijana waweze kujikomboa kiuchumi na kupunguza vijana wasio na ajira hapa nchini .

Benki hiyo ya  NMB  imekabidhi  mkopo huu kwenye hafla iliyofanyika katika  eneo la Benki ya NMB  tawi la Mpanda na Mgeni Maalum Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko alikabidhiwa mkopo huo wa bajaji  na pikipiki kwa walengwa.

Akizunngumza kwenye hafla hiyo  Meneja  mauzo wa NMB  Kanda ya Mgharibi  Trifon Melkiory alisema kuwa  Benki  ya NMB   imeanzisha mpango wa kuwakopesha waendesha bajaji na piki piki  kupitia mpango unaoitwa MASTABODA .

Amebainisha kuwa  mpango huo wa MASTABODA utawanufaisha  vijana wengi kiuchumi hapa nchini na kuwasaidia vijana wengine  kujiari  kwani kundi hilo  lina Idadi kubwa ya watu.

Melkiory amesema wametowa mkopo wa bajaji nane na pikipiki tatu zenye thamani ya shilingi Milioni 81,609,000,000 kwa ajili waendesha bajaji na boda boda  wa Mkoa wa Katavi waliokidhi vigezo vya kukopeshwa na Benki hiyo ya NMB.

Amefafanua kuwa Mkoa wa Katavi umekuwa wa kwanza kukopesha kiwango kikubwa cha fedha ukifuatiwa na Mkoa wa Tabora ambao wamekopeshwa hadi sasa jumla ya bajaji sita.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph amesema kuwa NMB  kwa kutowa mkopo huu wameiunga mkono Serikali  na wamepunguza tatizo la ajira  hivyo ni vema  vijana waitumie fursa  hiyo waliyopewa vizuri.

Mkuu wa Mkoa Katavi  Mwanamvua  Mrindoko  kwa upande wake aliwataka wananchi wa Mkoa wa Katavi kuhakikisha  wanachangamkia fursa  zinazo tolewa na benki ya NMB  kwa kujipatia mikopo ili kuweza kukuza uchumi wao na  wa Mkoa wa Katavi na nchi kwa ujumla .

Aliwasisitiza vijana hao  kuhakikisha wanakuwa na nidhamu   katika kurejesha  mikopo hiyo ya bajaji na boda boda  kwa kuzingatia masharti  ya mikopo ya Benki ya NMB  ili benki hiyo iendelee kuwaamini na wengine waweze kunufaika na mpango huu wa MASTABODA .

Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Haidary  Sumry alisema kuwa amefarijika sana kwa NMB kutoa mkopo huo kwani utasaidia hata mapato ya Manispaa ya Mpanda kuongezeka hivyo aliomba benki hiyo itowe tena mikopo hiyo na kwa vijana wengine .

Kwa  upande wake Mlezi wa  waendesha Bajaji na Boda boda  Mkoa wa Katavi Beda Katani  alisema kuwa vijana wa Mkoa wa Katavi wamepata fursa kubwa kutoka Benki ya NMB  kuliko Mikoa mingine hivyo waitumie vizuri fursa hiyo .

Tawi la Benki ya NMB Mpanda lililopo eneo la madukani Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi.


Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages