BENKI YA NMB YAWANOA WAFANYABIASHARA MKOA WA KATAVI

Wafanyabiashara wakiwa kwenye mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kufanya biashara zao kwa ufanisi yaliyotolewa na Benki ya NMB Mkoa wa Katavi


Na Walter Mguluchuma

      Katavi


Benki ya  NMB imewapatia mafunzo Wafanyabiashara wa Mkoa wa Katavi  yenye lengo la kuwajengea uwezo wa kufanya biashara zitakazo wanufaisha na kuwapatia wateja wa aina mbalimbali na kuinua kipato chao na uchumi wa Mkoa huo kwa ujumla.

 

Mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo wafanya biashara hao yamefanyika katika Ukumbi wa Manispaa ya Mpanda ulipo eneo la Kota za  Madini  na yaliwashirikisha Wafanyabiashara wote kutoka katika Wilaya zote za Mkoa wa Katavi.


Meneja wa Kanda  ya Magharibi wa Benki ya NMB Sospeter Magesse alisema kuwa  NMB wapo Katika Mkoa wa Katavi  kwa lengo la kuhakikisha  Wafanyabiashara wa aina zote wanakuza  biashara  zao na ndio maana wameamua kuwapatia mafunzo  yatakayo wanufaisha kwenye biashara zao mbalimbali wanazofanya .

 

Amebainisha kuwa wamekuwa wakitowa mikopo mbalimbali  kwa ajili ya kuwasaidia Wafanyabiashara na ndio maana wameanzisha pia mikopo ya wakulima na wafugaji , wavuvi,wachimbaji na wakandarasi  lengo ikiwa ni katika kumwinua Mfanyabiashara wa hali ya chini,wakati na wa hali ya juu.

 

Magesse aliongeza kuwa wao  NMB wanaimani kuwa mafunzo hayo waliowapatia Wafanyabiashara wa Mkoa wa Katavi  yatawasaidia  kuboresha  biashara zao na kuzikuza pia.

 

Upande wa sekta ya kilimo Benki hiyo ya NMB alieleza kuwa inakitengo  kinachoshughulikia na wanatowa mikopo kwa ajili ya zana za kilimo na ili mkulima aweze kukopeshwa zana za kilimo anatakiwa kuchangia asilimia 20 ya bei ya zana hizo.

 

Amefafanua kuwa mikopo hiyo pia hutolewa kwa kiwango hicho hicho kwa wateja wenye sifa za kukopesheka na wanaweza kukopa magari  zana za kuchimbia madini , mitambo ya ukandarasi ,bajaji,vifaa vya uvuvi  na vinginevyo .

 

Magesse amewataka Wafanyabiashara wa Mkoa wa Katavi kuwa na utaratibu wa kuweka bima za biashara zao kwani Wafanyabiashara wengi wa Mkoa wa Katavi biashara zao hazina bima .

 

Mwenyekiti  wa Business Club wa Mkoa wa Katavi Raymond Kamtoni  alieleza kuwa Wafanyabiashara wa Mkoa wa Katavi wamekuwa wakinufaika na Benki ya NMB kwa mikopo ambayo wamekuwa wakiwapatia ambapo kwa sasa riba imepunguzwa tofauti na Benki nyingine .

 

Alisema kuwa miongoni mwa Wafanyabiashara walionufaika na mkopo wa mitambo ya  kuchimbia dhahabu yeye ni mmoja wapo kwani  mtambo aliokopeshwa unamsaidia kwenye shughuli  zake na pia ameweza kuongeza ajira kwa vijana wanaofanya kazi kwenye mgodi wake .

 

Nae  Mwezeshaji wa mafunzo hayo  James Mwang'amba aliwasisitiza Wafanyabiashara kuweka fedha zao benki badala ya kuzihifadhi kwenye mitungi ndani ya nyumba zao  kwani wanapo weka fedha Benki inakuwa ni rahisi kuweza kukopesheka na Benki yoyote.

    

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages