MAHAKIMU WAPATIWA UELEWA JUU YA SHERIA ZILIZOREKEBISHWA .

Jaji  Mfawidhi wa Mahakama kuu Kanda ya Sumbawanga Jaji  Dustan Ndunguru  akifungua mafunzo yaliyowashirikisha  Mahakimu wa Mahakama zote zilizopo katika Mkoa wa Katavi  mafunzo hayo yakiwa na Lengo la kuwapatia uelewa wa sheria  mbalimbali zilizofanyiwa marekebisho(Picha na Walter MguIuchuma)


 Na Walteruluchuma

Mahakimu wa Mahakama za Mkoa wa Katavi wamepatiwa  mafunzo  ya uelewa wa pamoja kuhusu mabadiliko ya sheria mbalimbali zilizofanyiwa marekebisho ya sheria ya mwaka 2020 ili wawe na uelewa wa pamoja kwa kuwa wao ndio watumiaji wa sheria hizo.


Naibu Msajili wa Mahakama kuu Kanda ya Sumbawanga Maira  Kasonde   alisema kwa sasa Mahakama ipo kwenye kipindi cha maboresho  na moja ya mambo wanayoyafanya ni pamoja na kutoa  elimu kwa watumishi wake wa kada mbalimbali kuanzia Majaji na Mahakimu.


Alieleza baada ya sheria mbalimbali kufanyiwa marekebisho mwaka huu Uongozi wa Mahakama umeona ni vema Mahakimu wote wakapatiwa elimu  ya ulewa wa pamoja hivyo Mahakama kuu Kanda ya  Sumbawanga  imefanya  Uzinduzi wa mafunzo hayo katika Manispaa ya Mpanda Mkoani  Katavi na baada ya hapo watakwenda Wilaya ya  Nkasi , Kalambo na hatimaye Sumbawanga Mkoa wa Rukwa.


Lengo Kuu la mafunzo hayo likiwa ni kuhakikisha Mahakimu  ambao ni watumiaji wa sheria hizo wanakuwa na uelewa wa kutosha  na wapamoja  kuhusiana  na mabadiliko yaliyojitokeza huku sheria zilizofanyiwa marekebisho zikiwa ni nyingi na ambazo wameziona muhimu wazipitie na kuzifanyia mafunzo ni sheria tatu.


Sheria hizo tatu zilizofanyiwa marekebisho na wanazo zifanyia mafunzo Kasonde amezitaja kuwa ni  sheria  ya mwenendo wa makosa ya jinai  sura ya  20 kama ilivyorekebishwa mwaka 2019, sheria nyingine ni ya kanuni ya adhabu  sura ya 16  na sheria ya uhujumu uchumi ambayo nayo imefanyiwa marekebisho  kupitia sheria namba moja ya Mwaka 2020.


"...…tumeamua  kuwaita Mahakimu wote kwenye mafunzo hayo  wakiwemo Mahakimu wa Mahakama  za Mwanzo kwa sababu kuna sheria zinazotumika mahakama za juu pekee lakini siku hizo mahakimu wanao ajiliwa lazima waanzie  Mahakama ya Mwanzo ambapo hapo baadae huwa wanapanda hivyo ndio sababu tumeona washiriki Mahakimu wote ili  kesho na kesho kutwa wajuwe ni nini kinacho hitajika"alisema Naibu Msajili Kasonde.


Alifafanua kuwa  sheria  hizo zinatumika  pia  kwenye mahakama zote kama  vile sheria ya  kanuni ya adhabu inatumika pia katika Mahakama ya mwanzo na sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai  sura ya 20 kuna baadhi ya vipengele vinatumika katika Mahakama za mwanzo   na ambavyo vimeguswa  kikiwemo kifungu cha 91 cha sheria hiyo  kinacho mpa mamlaka DPP   Kuondoa shitaka Mahakamani  ndio maana wakaona watowe mafunzo kwa wote  ili wawe na uwelewa wa pamoja.


Katika hatua nyingine kwenye mafunzo hayo  mbali ya kuelimishana  wamejadili pia changamoto  zinazoibuka kuhusiana na sheria hizo na kuzipatia ufumbuzi  na mafunzo hayo yamefanyika  kutokana na maelekezo ya uongozi  wa juu wa  Mahakama.


Nae Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Katavi  Fred  Shayo amesema kuwa wamepitishwa kwenye mabadiliko mbalimbali ya sheria zilizorekebishwa mwezi Machi mwaka huu na kuzingatia sheria nyingi zinawahusu  Mahakama .

 

Hakimu Shayo alitolea mfano sheria ya  mabadilioko ya mwenendo wa makosa ya jinai  sura ya 20 toleo la mwaka 2022 imefanyiwa mabadiliko katika vifungu mbalimbali ikiwemo kifungu  namba 131 kinaelekeza kwamba mashauri yote yanayofunguliwa Mahakamani  lazima upelelezi uwe umekamilika  kama upelelezi utakuwa hauja kamilika mahakama inauwezo wa kufuta kesi hiyo ili kuepukana na mrundikano wa mashauri mahakamani .

 

Nae  Hakimu  David  Mbembele alisema kuwa marekebisho hayo ya  sheria yamezipa uwezo Mahakama za chini  kuwa na uwezo wa kutoa mdhamana  kwa kesi za uhujumu uchumi mpaka dhamani ya  chini ya shilingi milioni 300 ambapo hapo awali mahakama kuu ndio iliyokuwa na mamlaka hayo.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages