Na Walter Mguluchuma
Katavi .
Mkoa wa Katavi umefanikiwa kuyafikia maeneo yote ya muhimi kwa wakati ambayo watu walitakiwa kuhesabiwa kuanzia saa sita na dakika moja usiku yakiwepo maeneo ya stendi zote zate nyumba za kulala wageni ,bar.
Hospitalini .magereza. Watoto wa mitaani na kwenye treni ya abiria inayofanya safiri ya kutoka Mpanda kwenda Tabora .
Pia kwenye zoezi hilo la Sensa ya watu na Makazi linaloendelea kufanyika Mkoani Katavi hadi sasa hakuna changamoto ypyote ambayo imeisha jitokeza na wananchi wamehamasika sana na wanatowa ushirikiano mkubwa kwa makarani wa sensa .
Akizungumza na wandishi wa Habari mbele ya wananchi wa Mkoa wa Katavi Mwanavua Mrindoko kwenye maeneo mbalimbali aliyokuwa akiyatembelea katika Manispaa ya Mpanda wakati akikagua maendeleo ya zoezi la sensa alisema kuwamaeneo yote ya muhimu yameweza kufikiwa kwenye zoezi la sensa kwa wakati na na bila kuwepo kwa changamoto yoyote ile hadi sasa.
Amebainisha kuwa wananchi wa Mkoa wa Katavi wamehasika sana kwenye zoezi hili na wako tayari kuhesabiwa ambapo kwenye zoezi hili wananchi wamekuwa wakitowa ushirikiano mkubwa sana huku hali ikiwa ya maeneo yote ni salama .
Mrindoko alisema kuwa kwenye zoezi hilo wanahakikisha linafanikiwa kwa asilimia mia moja na watu wote wanafikiwa na kuhesabiwa kama ilivyokusudiwa bila kujali hali ya jografia ilivyo ya Mkoa huu.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi Haasan Abasi Rugwa amesema kuwa zoezi hili katika Mkoa wa Katavi limeanza kwa ufanisi mkubwa huku ulinzi na usalama ukiwa umeimalika na mpaka sasa hakuna malalamiko yoyote ya kutoka kwa wananchi kutokana kazi kubwa ambayo imefanywa ya zoezi la sensa kwenye Mkoa wa Katavi .
Hivyo amewataka kila wananchi wa Mkoa wa Katavi kuhakikisha anahesabiwa na ndio mkakati ambao Mkoa umejiwakea wa kuhakikisha hakuna mtu hata mmoja ambae hata hesabiwa kwenye zoezi hili .
Karani wa Senza wa eneo namba 002 huko katika eneo la Ilembo A siton Kajiba amesema kuwa zoezi hilo kwa upande wake limekuwa likienda vizuri kutokana na ushirikiano kutoka kwa wana wananchi kwani kila Kaya ambayo amekuwa akiifikia amekuwa amekuta wakiwa tayari wameandaa nyaraka muhimu zinazo hitajika kwenye zoezi hilo hali ambayo inaonyesha kuwa watu wamekuwa na uwelewa wa umuhimu wa sensa ya watu na makazi.