George Mwigulu na Erenest Kibada,Mlele.
Shirika lisilokuwa la Kiserikali la Association for the Development of Protected Areas (ADAP) Tanzania limeanza kusaidia Jumuiya ya wafuaga nyuki Inyonga kupitia vikundi vyake kusaidia kusindika uyoaga pori kwa njia ya kitalaam kwa kutumia Nishati ya Jua itakayokuwa ikitumia kifaa maalum kiitwacho Solar Draya,Jambo ambalo litasaidia vikundi hivyo kupata chakula na uchumi kuongezeka kwa kuuza uyoga pori huu.
Mzinga ukiwa shambani katika eneo la sshamba la ufugaji nyuki Msitu wa hifadhi ya Mlima Mlele ambapo mizinga hiyo inamilikiwa na Jumuiya ya wafuga nyuki ya Inyonga (IBA) |
Shirika lisilokuwa la Kiserikali la Association for the Development of Protected Areas (ADAP) Tanzania limeanza kusaidia Jumuiya ya wafuaga nyuki Inyonga kupitia vikundi vyake kusaidia kusindika uyoaga pori kwa njia ya kitalaam kwa kutumia Nishati ya Jua itakayokuwa ikitumia kifaa maalum kiitwacho Solar Draya,Jambo ambalo litasaidia vikundi hivyo kupata chakula na uchumi kuongezeka kwa kuuza uyoga pori huu.
Shirika hilo limekja na
mpango huo baada ya kuona wafugaji hao wanaofugia mizinga yao porini na lipo
zao la uyoga linaloharibika ambalo lingeweza kuwasaidia kwa chakula na
kuwaingizia kipato kwa kuwa uyoga pori ni muhmu kwa afya na unaprotini za
kutosha pamoja na vitamin katika mwili wa binadamu hasa kwa akinamama
wajawazito.
Hayo yamebainishwa
na Mkurugenzi wa ADAP) Tanzania DKT, Vicent Vyamana, wakati akizungumza
muda mfupi baada ya kutambulisha mradi wa uhifadhi Mazingira Utakaosaidia
vikundi vya wafuga nyuki katika wilaya ya MlelE, Nsimbo na Sikonge kisha
walitembelea eneo la ufugaji nyuki la Jumuiya ya wafugaji nyuki ya IBA
linaljumuisha vikundi vya wafuga nyuki na kujionea shughuli inayofanyika katika
eneo hilo.
Dkt Vyamana ameendelea
kueleza watanunua majokofu matatu ya kuanzia kwa ajili ya wafugaji wa nyuki
ambayo watayatumia kwa ajili ya kukaushia uyoga pori ambao ni Chakula
watakuwa wanauvuna kutoka katika mashamba yao ya kufugia nyuki kisha kukausha
na kuuhifadhi kwa ajili ya chakula na mwingine kuuza na kujipatia kipato.
Wakati
wakijishughulisha na ukaushaji wa uyoga na utundikaji mizinga uhifadhi wa
mazingira utakuwa ukiendelea kwa kuwa wanafundishwa kufunga nyuki na kuhifadhi
mazingira katika maeneo wanayofugia nyuki.
Awali Mwenyeikiti
wa Jumuiya ya wafuga nyuki kutoka kijiji cha Masigo Oscar Makolofila kwa
niaba ya wafuga nyuki alieleza baadhi ya changamoto mbalimbali zinazowakabili
ikiwemo ukosefu wa mitaji ya kuendeshea shughuli zao za ufugaji,ucheleweshwaji
kupatikana vibali vya kuingia porini maeneo wanakofugia nyuki
wanapotundika mizinga yao, kwani wanapoomba, vibali kutoka kwenye Mamlaka za
usimamzi wa Mistu hawapewa kwa wakati hali inayowafanya kutofanya kazi zao kwa
wakati kwa kuwa ulinaji nao unaendana na msimu..
Mwakilishi kutoka kutoka OR-TAMISEMI Idara ya Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali Dkt Masanja ameelekeza Halmashauri kuwasaidia wafugaji wa nyuki kwa kuwa mara nyingi miradi ya wafadhili huwa haiendelee pindi wanapoondoka na kuiacha miradi walioianzisha. Wafadhili wanawekeza fedha nyingi kwenye miradi lakini wanapoondoka mara miradi huwa haendelei.
Mkurugenzi wa ADA - Tanzania,Dk Vicent Nyamana akiwasiilisha mradi kwenye kikao cha wadau wa mazingira kilicofanyika ukumbi wa mikutano wa shule ya sekondari Inyonga. |
Dkt Masanja ameeleza mfano hapa wafadhili wameweka fedha nyingi kwenye mradi huo wa ufugaji nyuki kupitia Jumuiya hii ya wafuga nyuki ya IBA ,na iwapo wakiondoka mradi huu unaweza usiendelee.
“Nashauri Halmashauri
kuhakikisha wanawasapoti ili mradi huu uweze kuendelea kuwepo, na kuwanufaisha
wananchi”amesema Dkt Masanja.
Amewashauri Wafuga
Nyuki na kutumia fursa za Mikopo kutoka kwenye Halmadhauri
inayotolewa kupitia Mapato ya ndani waombe mikopo hii kwa kufuata taratibu
zilizowekwa watapatiwa ikiwemo kusajiri vikundi vyao mikopo ile haina riba
serikali ya inayoongozwa na Rais Mhe.Samia Suluhu Hassan inawajari wananchi
wake zipo fedha za kutosha kuwakopesha kupita kwenye Halmashauri zitummieni.
Katibu Tawala wilaya
Wilaya Mlele Lincolin Tamba akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya
Mlele Mhe Filberto Sanga wakati wa kikao cha kutambulisha mradi wa uhifadhi
mazingira amewataka wafadhili wanaotekeleza miradi kuweka uwazi ili kuondoa
sitofahamu kwa jamii na jamii nayo itoe ushirikiano kwa kuwa miradi hiyo ni ya
kwao.