JUMUIYA YA WAFUNGA NYUKI MLELE YAPIGWA TAFU.

Katibu wa IBA (pichani kashirikia notebook mkononi)Kalolo Charles akiongozana na wageni kutoka OR - TAMISEMI Idara inayoshughurikia mashirika yasiyokuwa ya kiserikali nchini na kutembelea shamba la nyuki.

George Mwigulu  na Erenest Kibada,Mlele.

Shirika lisilokuwa la Kiserikali la Association for the Development of Protected Areas (ADAP) Tanzania  limeanza kusaidia Jumuiya ya   wafuaga nyuki Inyonga kupitia vikundi vyake  kusaidia kusindika uyoaga pori kwa njia ya  kitalaam  kwa kutumia  Nishati ya Jua itakayokuwa ikitumia kifaa maalum kiitwacho Solar Draya,Jambo ambalo litasaidia vikundi hivyo  kupata chakula na uchumi kuongezeka kwa kuuza uyoga pori huu.

Mzinga ukiwa shambani katika eneo la sshamba la ufugaji nyuki Msitu  wa hifadhi ya Mlima Mlele ambapo mizinga hiyo inamilikiwa na Jumuiya ya wafuga nyuki ya Inyonga (IBA)

Shirika lisilokuwa la Kiserikali la Association for the Development of Protected Areas (ADAP) Tanzania  limeanza kusaidia Jumuiya ya   wafuaga nyuki Inyonga kupitia vikundi vyake  kusaidia kusindika uyoaga pori kwa njia ya  kitalaam  kwa kutumia  Nishati ya Jua itakayokuwa ikitumia kifaa maalum kiitwacho Solar Draya,Jambo ambalo litasaidia vikundi hivyo  kupata chakula na uchumi kuongezeka kwa kuuza uyoga pori huu.

Shirika hilo limekja na mpango huo baada ya kuona wafugaji hao wanaofugia mizinga yao porini na lipo zao la uyoga linaloharibika ambalo lingeweza kuwasaidia  kwa chakula na kuwaingizia kipato kwa kuwa uyoga pori ni muhmu kwa afya na unaprotini za kutosha  pamoja na vitamin katika mwili wa binadamu hasa kwa akinamama wajawazito.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa  ADAP) Tanzania DKT, Vicent Vyamana, wakati akizungumza muda mfupi baada ya kutambulisha mradi wa uhifadhi Mazingira Utakaosaidia vikundi vya wafuga nyuki  katika wilaya ya MlelE, Nsimbo na Sikonge kisha walitembelea eneo la ufugaji nyuki la Jumuiya ya wafugaji nyuki ya IBA linaljumuisha vikundi vya wafuga nyuki na kujionea shughuli inayofanyika katika eneo hilo.  

Dkt Vyamana ameendelea kueleza watanunua majokofu matatu ya kuanzia kwa ajili ya wafugaji wa nyuki ambayo watayatumia kwa ajili ya kukaushia uyoga pori ambao ni Chakula  watakuwa wanauvuna kutoka katika mashamba yao ya kufugia nyuki kisha kukausha na kuuhifadhi kwa ajili ya chakula na mwingine kuuza  na kujipatia kipato.

Wakati wakijishughulisha na ukaushaji wa uyoga na utundikaji mizinga  uhifadhi wa mazingira utakuwa ukiendelea kwa kuwa wanafundishwa kufunga nyuki na kuhifadhi mazingira katika maeneo wanayofugia nyuki.

Awali  Mwenyeikiti wa Jumuiya ya wafuga nyuki kutoka kijiji cha Masigo Oscar Makolofila  kwa niaba ya wafuga nyuki alieleza baadhi ya changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo ukosefu wa mitaji ya kuendeshea shughuli zao za ufugaji,ucheleweshwaji  kupatikana vibali vya kuingia porini maeneo wanakofugia nyuki wanapotundika mizinga yao, kwani wanapoomba, vibali kutoka kwenye Mamlaka za usimamzi wa Mistu hawapewa kwa wakati hali inayowafanya kutofanya kazi zao kwa wakati kwa kuwa ulinaji nao unaendana na msimu..

Mwakilishi kutoka kutoka OR-TAMISEMI Idara ya Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali Dkt Masanja ameelekeza Halmashauri  kuwasaidia wafugaji wa nyuki kwa kuwa mara nyingi miradi ya wafadhili huwa haiendelee pindi wanapoondoka na kuiacha miradi walioianzisha. Wafadhili  wanawekeza fedha nyingi kwenye miradi lakini wanapoondoka mara miradi huwa haendelei.

Mkurugenzi wa ADA - Tanzania,Dk Vicent Nyamana akiwasiilisha mradi kwenye kikao cha wadau wa   mazingira kilicofanyika ukumbi wa mikutano wa shule ya sekondari Inyonga.

Dkt Masanja ameeleza mfano hapa wafadhili wameweka fedha nyingi kwenye mradi huo wa ufugaji nyuki kupitia Jumuiya hii ya wafuga nyuki ya IBA ,na iwapo wakiondoka mradi huu unaweza usiendelee.

“Nashauri Halmashauri kuhakikisha wanawasapoti ili mradi huu uweze kuendelea kuwepo, na kuwanufaisha wananchi”amesema Dkt Masanja.

Amewashauri Wafuga Nyuki na   kutumia fursa za Mikopo kutoka kwenye Halmadhauri inayotolewa kupitia Mapato ya ndani waombe mikopo hii kwa kufuata taratibu zilizowekwa watapatiwa ikiwemo kusajiri vikundi vyao mikopo ile haina riba serikali ya inayoongozwa na Rais Mhe.Samia Suluhu Hassan inawajari wananchi wake zipo fedha za kutosha kuwakopesha kupita kwenye Halmashauri zitummieni.

Katibu Tawala wilaya Wilaya Mlele Lincolin Tamba akizungumza  kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Mlele Mhe Filberto Sanga wakati wa kikao cha kutambulisha mradi wa uhifadhi mazingira amewataka wafadhili wanaotekeleza miradi kuweka uwazi ili kuondoa sitofahamu kwa jamii na jamii nayo itoe ushirikiano kwa kuwa miradi hiyo ni ya kwao.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages