KAMATI YA USHAURI YATOA TAMKO LA KUTORIDHISHWA NA KASI UMEME WA GRIDI YA TAIFA.

 

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akizungumza namna ambavyo hajaridhishwa na utekelezwaji wa mradi ya umeme wa Gridi ya Taifa.

Na Walter Mguluchuma,Katavi.

KAMATI  ya ushauri ya Mkoa wa Katavi  imetoa tamko la kutoridhishwa na kasi  ya ujenzi wa umeme wa  gridi ya Taifa unao tokea  Mkoani Tabora  kuwa haidhishi hata kidogo wakati wananchi wanahitaji umeme.

Kamati  ya ushauri ya Mkoa wa Katavi  imetoa tamko la kutoridhishwa na kasi  ya ujenzi wa umeme wa  gridi ya Taifa unao tokea  Mkoani Tabora  kuwa haidhishi hata kidogo wakati wananchi wanahitaji umeme

Tamko hilo limetolewa wakati wa kikao hicho  kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda kilichoongozwa na Mkuu  wa Mkoa wa Katavi Mwanavua Mrindoko .

Azimio la tamko hilo limetolewa  na wajumbe wa kikao hicho kufuatia taarifa iliyotolewa mbele ya wajumbe wa kikao hicho na  Afisa mahusiano wa  Tanesco Mkoa wa Katavi  Proches  Joseph kuwa mradi huo unatarajia kukamilika ifikapo mwezi wa Agosti mwakani na kwa sasa umefikia asilimia  20 .3 upo kwenye usafishaji wa njia za kuweka nguzo na kusambaza .

Kufuatia kutolewa kwa taarifa hiyo Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Mwanamvua Mrindoko  ameeleza kutoridhishwa  na utekelezaji  ujenzi   wa  mradi  wa  umeme  wa Gridi   ya Taifa  Mkoani Katavi  kutokana na kususua  utekelezaji wa mradi huo .

Amesema  kuwa  kasi ya  ujenzi  wa  mradi  huo  imekuwa  ndogo  isiyoridhisha  kwa  kwa kuwa mpaka sasa  mradi huo umetekelezwa kwa ailimia 20.3

Amesema kuwa wakati wa ziara ya Makamu wa Rais aliyoifanya Mkoani Katavi aliagiza kuwa mradi huu ukamilike kwa wakati  uliopangwa  ili wananchi wa Mkoa wa Katavi  waweze kupata umeme wa uhakika

Mbunge wa jimbo la Mpanda  Vijijini  Moshi Kakoso  akisema kuwa tatizo la mradi wa umeme sio la gridi ya Taifa hata kwenye   mpango wa Rea  awamu ya tatu kasi ni ndogo kwani unatakiwa kukamilika mwezi wa tatu mwakani lakini hadi sasa ni vijiji  9 tuu walivyoweka umeme katika

Mkoa mzima kati ya vijiji 52 vya Mkoa huu vinavyotakiwa kupatiwa umeme  kwenye aamu hiyo .

Mbunge wa jimbo la Mpanda Mjini  Sebastian  Kapufi alieleza kuwa kasi ya ujenzi wa umeme wa gridi ya Taifa sio ya kuridhisha kwani kinachoinekana kwenye mradi huo ni njia tuu za   sehemu watakazo pitisha umeme na nguzo zilizo rundikwa .

Ameshauri kuwa  badala ya kuweka nguzo  za umeme kwenye mradi huo za miti  wangeweka nguzo za zege  kwani inashangaza   maeneo ya mijini huko wanawake nguzo za zege  na  kwenye mradi huu unaopita maeneo ya pori wanaweke nguzo za miti ambazo muda wowote zinawza kuungua kwa moto au kuangushwa na wanyama kama tembo .

Wajumbe wa kikao hicho baada ya kuwa wamepokea michango ya wajumbe mbalimbali walitowa taamko la kutoridhishwa na kasi ya ujenzi wa mradi huo na kuzishauri mamlaka husika kufatilia ujenzi wa mradi huo.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages