MBUNGE KAPUFI AHIMIZA MAFUNZO KWA WACHIMBAJI MADINI.

Baadhi ya washiriki wa kikao cha kamati ya Mkoa wa Katavi (RCC) wakiwa kwenye kikao cha kamati hiyo wakijadiliana mambo mbalimbali ya maendeleo ya Mkoa wa Katavi na Taifa kwa ujumla. 
(Picha na Walter Mguluchuma)

Na Walter Mguluchuma,Katavi.

MBUNGE  wa Jimbo la Mpanda Mjini  Sebastian Kapufi   ameomba wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu  wawekewe na Serikali utaratibu wa kupatiwa mafunzo  ya uchimbaji  bora wa madini hayo  ili waweze kupata uwelewa zaidi utakao wafanya wawe na uchimbaji bora kuliko ilivyo sasa.

Mbunge wa viti Maalumu Mkoa wa Katavi Tasca Mbogo  akitowa mchango wake wa  maswala mbalimbali yanayohusu maswala ya Maendeleo ya Mkoa wa Katavi na Nchi kwa ujumla wakati wa kikao cha kamati ya ushauri ya Mkoa wa Katavi kilichofanyika katika ukumbi wa  Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda ambapo amewashauri maafisa ardhi wanapo panga mipango miji wasiangalie tuu vizazi vya sasa  bali wapange miji na kwa kuzingatia vizazi vijavyo. (Picha na Walter Mguluchuma)

Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini  Sebastian Kapufi   ameomba wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu  wawekewe na Serikali utaratibu wa kupatiwa mafunzo  ya uchimbaji  bora wa madini hayo  ili waweze kupata uwelewa zaidi utakao wafanya wawe na uchimbaji bora kuliko ilivyo sasa.

Ombi hilo ametowa wakati wa kikao cha kamati ya ushauri ya Mkoa wa Katavi (RCC) kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Mpanda kilichojadili mambo mbali mbali ya maendeleo yanayohusu Mkoa huu na Taifa kwa jumla .

Amebainisha  kuwa kumekuwepo na utaratibu kwenye sekta nyingine kama kilimo  kuwa  wanapatiwa wakulima  elimu ya uzalishaji bora wa mazao yao lakini jambo hilo limekuwa halifanyiki kwa wachimbaji wadogo wa madi ya dhahabu ambao ni sehemu kubwa ya  waongezaji wa pato la Taifa na ajirakwa watu .

Hivyo ameomba Serikali iwaangalie wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu wa Mkoa wa Katavi na wamikoa mingine  kunakofanyika  shughuli za uchimbaji wa madini unaofanywa na wachimbaji wadogo  waweze kupatiwa elimu  ya uchimbaji ulio bora .

Kapufi amefafanua kuwa  mchimbaji mmoja  akipatiwa  uwezo wa uchimbaji ulio bora  atakuwa na uwezo mkubwa sana  wa kuongeza ajira kwenye  nyanja nyingine ndani ya Mkoa huu wa Katavi na nje ya Mkoa .

Ameeleza kuwa kutokana na elimu  ya uchimbaji bora ambayo atakuwa amepatiwa mchimbaji inamfanya aongeza  kiwango cha madini anayochimba na  kumfanya pia aweze kuongeza ajira kwenye sekta  nyingine kwani anaweza kuajiri watu  hata kwenye kilimo na kwenye sekta  nyingine kutokana    na miradi mingine ambayo atakayo kuwa ameianzisha  kutokana na mauzo ya madini  aliyoyauza.

Kuhusu   maswala ya afya amesema kuwa  ukamilishwaj ujenzi i wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi inayotalajiwa kuanza kazi mwezi Desemba mwaka huu itakuwa ndio mwarobaini  kwa  wananchi wa Mkoa wa Katavi .

Hivyo amesisitiza kuwa kwa watumishi wa afya watakao kuwa  wanatowa huduma kwenye Hospitali hiyo wanatakiwa kuwa na lugha nzuri kwa wagonjwa kwani ukimpa mgonjwa lugha nzuri  inakuwa ni sawa na  kumpatia tiba mgonjwa .

Mbunge wa viti maalumu Mkoa wa Katavi Tasca Mbogo  amesema kuwa umefika wakati wa kuangalia namna ya kupunguza  na kutatua tatizo la upungufu wa walimu katika Mkoa wa Katavi kwani hadi sasa kunajumla ya upungufu wa walimu  wa shule za msingi na Sekondari 3,243 katika Mkoa huu.

Ameshauri pia  maafisa ardhi  wanapo panga  miji  wasiangalia hali ya vizazi vya sasa  mbali  wawe wanaangalia na hali ya vizazi vinavyo kuja kwani kumekuwepo na tabia ya maafisa hao kupanga miji kwa kuangalia tuu hali ya sasa tuu bila kuangalia hali ijayo .

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko kwa upande wake  amesema kuwa Mkoa wa Katavi ni ghala la chakula  hivyo wananchi wa Mkoa huu waendelee kutumia vizuri  mvua  zinazo endelea kunyesha .

Amewataka wanachi  waendelee  kufanya kazi  na kuboresha uchumi wao kwani  kilimo ni biashara  ,hivyoaliwaagiza Wakuu wa Wilaya katika Mkoa huu wahakikishe mbolea ya ruzuku inafika kwa wakati kwa wakulima na bila  kuhujumiwa na mtu yetote.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages