TANROAD KATAVI KUTUMIA ZAIDI YA BILIONI 17 KUTENGENEZA BARABARA

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akifungua kikao cha Bodi ya barabara ambapo amesema sekta ya barabara katika mkoa huo umepiga hatua kwnye masuala ua usafuru na usafirishaji kutokana na kuwa na barabara zenye kiwango bora. (Picha na Walter Mguluchuma)

Na Walter Mguluchuma,Katavi.

ZAIDI  ya shilingi Bilioni 17 zimetengwa  kwa ajiri ya matengenezo ya barabara zinazosimamiwa na TANROADS Mkoa wa Katavi katika  kipindi cha bajeti ya mwaka wa fedha wa 2022/2023 huko Zaidi ya shilingi Bilioni  12 zikitoka katika mfuko wa barabara na Zaidi ya Bilioni  4 kutoka mfuko wa maendeleo  wa barabara.

Meneja wa TANROAD Mkoa wa Katavi,Mwandisi Martin Mwakabende akitoa taarifa ya utendaji kazi TANROAD ndani ya mkoa huo mbele ya Wajumbe wa bodi ya  barabara katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda Mkoani humo (Picha na Walter Mguluchuma)

Zaidi ya shilingi Bilioni 17 zimetengwa  kwa ajiri ya matengenezo ya barabara zinazosimamiwa na TANROADS Mkoa wa Katavi katika  kipindi cha bajeti yam waka wa fedha wa 2022/2023 huko Zaidi ya shilingi Bilioni  12 zikitoka katika mfuko wa barabara na Zaidi ya Bilioni  4 kutoka mfuko wa maendeleo  wa barabara

Hayo yameelezwa na Meneja wa TANROADS  wa Mkoa wa Katavi Mwandisi Martin Mwakabende wakati alipokuwa akitowa taarifa ya utendaji kazi wa TANROADS Mkoa wa Katavi kwenye kikao cha Bodi ya Barabara kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Mpanda kilichoongozwa na Mkuu wa Katavi Mwanamvua Mrindoko ambae  alikuwa mwenyekiti wa kikao hicho.

Mwakabende ameeleza kuwa  jumla ya shilingi Bilioni 17.254 zimetengwa kwa ajiri ya matengenezo ya   barabara  huku katika ya fedha hizo  kiasi cha shilingi Bilioni  12. 743 ni za kutoka katika mfuko wa barabara na kiasi cha shilingi Bilioni 4. 511 ni za kutoka katika  mfuko wa maendeleo .

Katika mwaka huu wa fedha Mkoa  Mkoa umepanga  kutekeleza miradi 39 yenye thamani  ya jumla ya shilingi   Bilioni 12, 743,441 kwa ajiri ya  kufanya matengenezo  ya Barabara kuu za Mkoa  zenye jumla ya kilometa 1,201 .81pamoja na kufanya  matengenezo ya  kinga katika madaraja  201.

Baadhi ya Wajumbe wa kikao cha bodi ya barabara Mkoa wa Katavi wakifuatilia kikao hicho kwa makini wakati kikifanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi.
 (Picha na Walter Mguluchuma)

Kwa upande wa fedha za maendeleo  wamepangiwa  jumla ya shilingi Bilioni  4.511ambapo kati ya fedha hizo  milioni  947 ni  kutoka  Bodi ya barabara  ni kwa ajiri  ya ukarabati  wa  Mkoa  na Wilaya zenye  urefu wakilometa  19.5 na Bilioni 3.564 ni za kutoka  mfuko wa maendeleo  ambazo zitakuwa kwa ajiri ya  ukarabati wa barabara  zaMkoa  na Wilaya zenye urefu wa kilometa  65.4

Mwandisi Mwakabende amebainisha kuwa  hadi kufikia  Novemba 2022  mikataba 39 imekwisha sainiwa tayari  na mikataba hiyo  imeisha pata msamaha wa kodi  na kazi za matengenezo ya barabara  zimeanza kutekelezwa .

Amezitaja baadhi ya changamoto  zilizopo katika utekelezaji wa kazi zao  kuwa ni wananchi  kupitisha  mifugo  barabarani  hivyo  huchangia  kwa kiasi kikubwa  uharibifu wa barabara ,wananchi  kufanya shughuli  za kilimo  ndani ya maeneo  ya hifadhi  ya barabara kama vile  barabara ya  Kagwira  kwenda Karema mwambao mwa ZiwaTanganyika .

Changamoto nyingine ameitaja kuwa ni  uhaba wa  upatikanaji wa kifusi  kwa barabara  zinazopita  ndani  ya  maeneo ya Hifadhi ya Taifa ya Katavi sharia  ya hifadhi hairuhusu  kuchukua kifusi katika hifadhi  aliomba kama  kuna  uwezekana wa TANROADS kuondokana na changamoto hiyo  barabara  hizo zihudumiwe na Hifadhi zaTaifa .

Amesema baada ya  kufanyika kwa matengenezo  ya barabara za Mkoa huu na zinazounganisha  na mikoa mingine na Wilaya na Wilaya  na kuwa na barabara zenye unafuu huduma ya mabasi  imeongezeka  pamoja na nauli kupungua .

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanavua Mrindoko amewaeleza wajumbe wa kikao hicho kuwa Mkoa wa Katavi  umefanikiwa sana  kwenye maswala ya sekta ya barabara  kwa upande wa usafiri  na uchukuzi  kwani Serikali  imeendelea  kutenga  bajeti  na kutekeleza kwa kiwango kikubwa.


Mbunge wa jimbo la Mpanda mjini Mkoa wa Katavi,Sebastian Kapufi akiwa na Mbunge wa viti maalumu wakifuatilia kwa makini kikao cha bodi ya barabara kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda Mkoani humo. (Picha na Walter Mguluchuma)

Hali hiyo imeufanya  mkoa wa Katavi kuwa  na mabadiliko makubwa sana kwenye sekta ya barabara na kuufanya  kufika kwa urahisi Zaidi  kupitia barabara zote zinazounganisha mkoa huo na mikoa mingine pamoja nan chi za Kongo na Burundi.

Mbunge wa jimbo la Mpanda Mjini  Sebastian Kapufi  ameomba fedha zinazotolewa na Serikali zinazotokana na tozo kwa ajiri ya barabara zinazosimamiwa na TARURA zigawanywe kwa usawa kwa kila Halmashauri  wasiangalie kama kuna miradi mingine ya wafadhili inayotekelezwa kwenye  Halmashauri nyingine .

Amesema katika fedha za tozo zilizopelekwa kwenye halmashauri za Mkoa huu ni Halmashauri yake pekee ya Manispaa ya Mpanda iliyopewa kiasi cha shilingi  bilioni moja  wakati Halmashauri nyingine za  mkoa huu walipatiwa kiasi cha shingi bilioni moja na nusu sababu ya Halmashauri yake kuwa fedha ndogo ilidaiwa ni kwa kuwa  wanayo miradi mingine jambo ambalo sio sawa kwani kadi wananchi wote wanatozwa sawa sawa bila kujali wa halmashauri ipi.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages