Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini,Sebastian Kapufi (Kwaza kushoto) akikabidhi mahitaji mbalimbali kwa Kaimu Mkuu wa Gereza la Mahabusu Mpanda,Christopher Fungo. |
Walter Mguluchuma na Paul
Mathias.
Kaimu Mkuu wa Gereza Mahabusu la Mpanda amemshukuru Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini Sebastiani Kapufi kwa kuguswa na kuona kushirika katika mwaka mpya kwa kushiriki na Jamii iliyotegwa kwa Mjibu wa sheria na jamii waliohukumiwa na wengine wakisubilia vifungo vyao kwa kuwapatia Mahitaji mbalimbali ikiwemo Chakula.
Kaimu
Mkuu wa Gereza Mahabusu la Mpanda amemshukuru Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini
Sebastiani Kapufi kwa kuguswa na kuona kushirika katika mwaka mpya kwa kushiriki na Jamii
iliyotegwa kwa Mjibu wa sheria na jamii waliohukumiwa na wengine wakisubilia
vifungo vyao kwa kuwapatia Mahitaji mbalimbali ikiwemo Chakula.Kaimu Mkuu wa Gereza la Mahabusu Mpanda,Christopher Fungo akitoa shukrani kwa Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini,Sebastian Kapufi baada ya kukabidhiwa mahitaji mbalimbali.
Shukurani
hizo zimetolewa na Kaimu mkuu wa Gereza la mahabusu Mpanda Christpher Fungo
mara baada ya kupokea msaada huo aliokabidhiwa na Mbunge wa Jimbo la Mpanda
mjini Sebastiani Kapufi.
Alisema kuwa
bado wanaendelea kuhitaji misaada mingine na tunashukuru kwa kuguswa na
kutambua kuwa wenzetu hawa wanahitaji vitu kama hivyo.
Ameeleza kuwa mbunge huyo amejinyima kwa moyo wa dhati kwa kujitolea kwa niaba ya watumishi wa magereza anaomba msaada huo usiishie hapo bali uwe endelevu kwao.
Kwa pande wake Mbunge wa Jimbo la Mpanda mjini Sebastiani Kapufi amesema ameguswa kwa kuamini kuna wenzetu wa Magereza na watoto yatima kwa namna ambayo mwenyezi mungu amemjalia na wakati tukienda kuupokea mwaka mpya 2023 amewiwa kuwatembelea na kutoa vitu mbalilmbali.
Alisema ametoa zawadi ya Vitu mbalimbali ikiwemo Mafuta ya Kupikia, Sabuni ,Mchele, Taulo za kike,Dawa za meno ,Nyama ya Ng’ombe na Vinywaji baridi.
Moses Mbesella Mkuu wa Gereza la Mahabusu Mpanda anaemaliza utumishi wake wa umma akitoa maneno ya shukrani. |
Ameeleza kuwa mbunge huyo amekuwa mbunge wa muda mrefu na analijali sana Gereza la Mahabusu Mpanda na tunamwombea kwa mwenyezi mungu aendelee kumujalia moyo wa ukalimu alisema Moses.