WATOTO YATIMA WASHUKURU KWA MIKONO MIWILI MSAADA WA MBUNGE KAPUFI.


Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini,Sebastian Kapufi (kushoto) akisalimiana na Sister Rose Sungura.

Na Walter Mguluchuma,Mpanda.

Watoto yatima waliopo katika kituo cha kulea watoto cha Mtakatifu Yohane Paul wa pili Matumaini ya watoto kilichopo Manispaa ya Mpanda  mkoa wa katavi wameshukuru Msaada ulitoewa na Mbunge wa jimbo la Mpanda Mjini Sebastiani Kapufi kwaajili ya sikukuu ya mwaka mpya.

Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini,Sebastian Kapufi akizungumza na waandishi wa habaei mara baada ya kumaliza kutoa mahitaji mbalimbali.

Watoto yatima waliopo katika kituo cha kulea watoto cha Mtakatifu Yohane Paul wa pili Matumaini ya watoto kilichopo Manispaa ya Mpanda  mkoa wa katavi wameshukuru Msaada ulitoewa na Mbunge wa jimbo la Mpanda Mjini Sebastiani Kapufi kwaajili ya sikukuu ya mwaka mpya.

Akipokea zawadi hizo kwa niaba ya watoto hao Mkuu wa kituo hicho Sisiter Rose Sungura amesema wamepokea zawadi ya vitumbambali kutoka kwa Mbunge huyo  kwa mikono miwili.

Amesema kuwa kituo hicho  kilianzishwa mwaka 2019 na Mpaka sasa kimeshapokea jumla ya Watoto 50 ambapo watoto walipo kwa sasa kituoni hapo ni watoto 21.

Kituo hicho kimeanza kukua hii inatokana na mapokea mazuri ya Jamii ya watu wa Mpanda kwa kuendelea kukilea na kukitunza kituo hicho na mungu awabariki sana.

Amesema mbunge huyo ametenda tendo jema sana na mungu amemuona na aendelee kuwaona watu wake wa Mpanda kwa kama jinsi alivyowaona watoto hao.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini Sebastiani Kapufi ameguswa kwa kuamini kuna watoto yatima na magereza kwa kuwapatia chakula na mahitaji ya vitu vingine.

Amebainisha kuwa alipokuwa Magereza ameobwa afikishe salamu zake za upendo kwa umma kuwa kuwa Gerezani siomwisho wa maisha na eneo hilo mtuyeyote anaweza akafika huko.

Kubwa walilomweleza wanasema wataendelea kuwa watu wema na hata wao wanaweza wakawa wabunge watalajiwa na wameomba watakapomaliza kifungo chao jamii iwapokee kwakuwa watakua wameshakuwa watu wema.

Ukiacha wafugwa kuna watoto yatima ambapo amefika hapo na kuwasaidia mahitaji kidogo aliyojaliwa na mwenyezi Mungu kwa kuwapatia Pampas,Maziwa ya kopo lactrogen,Mchele na mafuta ya Mawese pamoja na nyama.

Pamoja na kutoa msaada kwa Magereza na wafungwa na kituo cha watoto cha mtakatifu Yohane anatalajia kutembelea hospitali ya rufaa ya mkoa wa katavi na kuwafariji wagojwa kwa kuwapatia vitu mbalimbali. 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages