RC KATAVI : 9 JANUARY SIO SIKU YA MWALIMU MKUU KUHANGAIKA KUPANGA MADAWITI.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akizungumza na wananchi wa mtaa wa Nsemlwa Manispaa ya Mpanda Mkoani hapo wakati akikabidhiwa vyumba vya madarasa (Picha na George Mwigulu)

Paul Mathias,Mpanda.

Serikali ya Mkoa wa Katavi imesema haita mvumilia mzazi au mlezi atakae onyesha kikwazo kwa wanafunzi waliofaulu kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2023 kwa kuwa serikali imeendelea kuboresha Mazingira ya elimu ndani ya Mkoa wa Katavi.

Mwanamvua Mrindoko,Mkuu wa Mkoa wa Katavi akikata utepe kuashiria kuyapokea vyumba vya madarasa katika shule ya sekondari Lyamba Manispaa ya Mpanda (Picha na George Mwigulu)

Serikali ya Mkoa wa Katavi imesema haita mvumilia mzazi au mlezi atakae onyesha kikwazo kwa wanafunzi waliofaulu kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2023 kwa kuwaserikali imeendelea kuboresha Mazingira ya elimu ndani ya Mkoa wa Katavi.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko wakati akikabidhiwa Madarasa 119 yaliyojengwa kwa fedha zilizotolewa na Rais Dk Samia Suluhu Hassani kwenye hafla iliyofanyika Shule ya Sekondary Lyamba Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi.

Mwanamvua amesema Mkoa wa katavi ulipokea kiasi cha shiligi Bilioni 2 na milioni 380 kwaajili ya ujenzi wa Vyumba vya Mdarasa 119 katika Mkoa wa katavi.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindiko (mbele kushoto) akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Mpanda,Sophia Kumbuli baada ya kumaliza kufanya ukaguzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Sekondari Mpanda Day (Picha na George Mwigulu)

Amesema madarasa hayo yamekamilika na yapo tayari kuwapokea wanafunzi wa Kidato cha kwanza mwaka 2023 ambapo Halmashauri ya manispaa ya Mpanda imefakiwa kujenga Vyumba vya Madarasa 51 vyenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.2

Amesema mwaka 2022 wanafunzi 14,904 wamefaulu kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka 2023 sawa na 84% kwa Mkoa wa Katavi.

Katika hatua nyingine amefafanua wazazi serikali haitakuwa na saliamtume kwa mzazi au mlezi atakaeonyesha kikwazo kwa Mtoto alimefaulu kujiunga Kidato cha kwanza na hatua kali za kisheria kwa yeyote atakaebainika kukwamisha maendeleo ya watoto kulipoti Shuleni kujiunga na kidato cha Kwanza.

Mwanamvua amewasihi watendaji wa Serikali katika mkoa wa katavi Kuendelea kushirikiana katika kumsaidia Rais Dk Samia Suluhu Hassan Kwenye usimamizi wa fedha za maendeleo zinazo letwa na serikali ili ziweze kutoa matokea yanayotalajiwa kwa wananchi na serikali kwa ujumla.

Awali akisoma taarifa ya ujenzi wa madarasa katika Manispaa ya Mpanda,Mkrugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Sophia Kumbuli amesema kuwa Jumla ya wanafunzi 4186 sawa na 86% wamefaulu kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2023 na vyumba vya Madarasa vimekamilika kwaajili ya kuwapokea wanafunzi hao katika halmsahuri ya manispaa ya Mpanda.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi,Sophia Kumbuli akisoma taarifa mbele ya Mkuu wa  Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko wakati wa kukabidhi vymba vya madarasa 51 katika Manispaa hiyo (Picha na George M wigulu)

Muonekano wa vyumba vya madarasa katika shule ya sekondari Lyamba Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi.(Na George Mwigulu)

Mwonekana wa ndani wa vyumba vya madarasa unaonesha ambao katika shule ya sekondari Mpanda Day Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi.(Na George M\wigulu)

Mwonekano wa vyumba vya madarasa katika shule ya sekondari Lyamba Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi (Picha na George Mwigulu)



Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko (kushoto) akiwa ameketi kwenye moja ya vyumba vya madarasa katika shule ya sekondari Lyamba (Picha na George Mwigulu)

Amewaasa wazazi kuhakikisha wanaanza kufanya Maandalizi mapema ya watoto wao kwaajili ya kujiunga na Kidato cha kwanza Mwaka 2023.

Baadhi ya wananchi waliohudhuria katika hafla hiyo akiwemo Said Juma amesema kuwa wanaishukuru serikali kwa kuendelea kuboresha mazingira ya Elimu na kumpongeza Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuja na Mpango wa kujenga vyumba vya Mdarasa kwaajili ya wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2023.

Helemani Mlowe mkazi wa Manispaa ya Mpanda akiwa katika hafla hiyo amesema kwa kipindi cha nyuma walikuwa wanahangaika sana watoto wao kusafiri umbali mlefu kwenda shuleni lakini kwa ujenzi huo wa Mdarasa utawafanya wanafunzi kuongeza jitihada katika masomo yao.

Kukamilika kwa Ujenzi wa Vyumba vya Mdarasa 119 katika mkoa wa Katavi kutawafanya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha kwanza mwaka 2023 kuchaguliwa kuanza masomo kwa awamu Moja.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages