TAKUKURU YAMFIKISHA MAHAKAMANI MKURUGENZI MUWASA BAADA YA AGIZO LA WAZIRI MKUU


Mahakama ya Wilaya ya Mpanda.

Na Walter Mguluchuma,Katavi

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Katavi imemfikisha Kizimbani Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira wa Manispaa ya Mpanda(MUWASA) Hussein Salumu  Nyemba ambae  Waziri Mkuu aliiangiza Takukuru kumfanyia uchunguzi.

Mkurugenzi wa MUWASA Mpanda - Hussain Nyemba (mbele)akiwa na Justine Wambali kaimu Afiisa Utumishi MUWASA wakifikishwa  mahakamani.

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Katavi imemfikisha Kizimbani Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira wa Manispaa ya Mpanda(MUWASA) Hussein Salumu  Nyemba ambae  Waziri Mkuu aliiangiza Takukuru kumfanyia uchunguzi

Kaimu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi  Stuart Kiondo amewaambia wandishi  kuwa mtuhumiwa huyo amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya  Mpanda akiwa na mtuhumiwa mwingine KaimuAfisa Utumishi wa( MUWASA )  Justine  Wambali mbele ya Hakimu Mkazi  mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Gaspher Luoga.

Mkurugenzi wa MUWASA Mpanda - Hussain Nyemba.

Watuhumiwahao wamesomewa mashita mawili kila mmoja ambapo shitaka la kwanza wameshitakiwa  kwa kosa  kutumia vibaya madaraka na shitaka la pili wameshitakiwa kwa kosa la kuisababishia MUWASA  hasara ya Tshs 17,817,000. Kinyume na kifungu cha sharia   namba 284A(1) sura ya 16 marejeo ya  2022 na kifungu  cha sharia Namba  57(1) na 60 (2) cha sharia ya uhujumi uchumi  sura namba 200 marejeo yam waka 2022.

Amesemamnamo tarehe 12 mwezi wa 12,    2022 Waziri  Mkuu Kassimu Majaliwa  alipokuwa kwenye ukumbi wa Manispaa ya Mpanda alipokuwa akiongea na watumishi  alitowa maelekezo kwa Takukuru kufanya uchunguzi kwa Hussen Nyemba  ambae ni Mkurugenzi wa  Mamlaka ya Maji safi na usafi waMazingirawa Manispaa ya Mpanda (MUWASA)

Katika  uchunguzi uliofanywa na Takukuru Mkoa wa Katavi wamewezakubaini kuwa watuhumiwa  hao wote wawili wanahusika juu ya tuhuma hizo mbili  hari ambayo imewafanya Takukuru kuwafikisha Mahakamani

Kaimu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi,Stuart Kiondo akitoa taarifa kwa wananhabari ya kufikishwa mahakamani Mkurugenzi wa MUWASA.

Kaimu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi  Stuart Kiondo  alieleza kuwamaelekezo ya Waziri Mkuu ilikuwa ni kumfanyia uchunguzi Hussein  Nyemba  lakini  Justine Wambali amejuishwa kwenye kesi hiyo kwa kuwa  yeye ni Kaimu  Afisa utumishi  anawajibika kwani yeye kwa nafasi yake alishindwa kumshauri Mkurugenzi wake na kuajiri watumishi 37 bila kufuata utaratibu na kuisababishia MUWASA kiasi hicho cha fedha .

Amesema  Mkurugenzi huyo  amefanikiwa kutimiza mashariti ya mdhamana  Mahakamani hapo ambapomashariti ya mdhamana kwenye kesi hiyo ilikuwa kila mtu mmoja  awe na mdhamini mwenye mali isiyo hamishika yenye thamani ya shilingi milioni tano na barua kutoka kwenye mamlaka zinazotambulika na Serikali  .

Hata hivyo mtuhumiwa Justine Wambali bado anaendelea kutafuta dhamana hadi muda wa kuhailishwa kwa kesi alikuwa  bado haja timiza mashariti ya  mdhamana Mahakamani hapo .

Kiondo amewaasa watumishi kufanya kazi kwa kuzingatia  maadili ya kazi zao  kwa sasabu wasipo zingatia maadili upo uwezekano wa kutokea mambo kama hayo  pia wakuu wa Taasisisi za umma  kwa Mkoa wa Katavi katika utendaji kazi wao wa kila siku wazingatie sharia na maadili    na wawe mfano kwa watumishi wao wanao waongoza  isitoke jambo kama hili kiongozi wa taasisi kuwa yeye ndie anae husika .

Kaimu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi amewaomba wananchi kuendelea kutowa ushirikiano kwa Takukuru ilikuweza kusaidia Mkoa wa Katavi ambao  upochini kwa maswala ya Rushwa

Ushirikiano huu pia uwepo kwenye  miradi ya Maendeleo  miradi ya maendeleo inaletewa fedha nyingi na Rais Dkt Samia  Suluhu Hassan  fedha nyingi zinaletwa kwenye mabarabara ,madarasana  kwenye sekta nyingine  kwa hiyo washirikiane pale pindi wanapoona kuna matatizo kwenye miradi hiyo ili waweze kufatilia kwani miradi hiyo ni mali yao wananchi .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages