WAZIRI MKUU ARIDHISHWA NA UBORA WA BARABARA MLELE

 

Waziri Mkuu Kassim  Majaliwa akiwahutubia wakazi wa Halmashauri ya Mlele katika Kijiji cha Mapili mara baada ya kukagua barabara

Na Walter Mguluchuma,Mlele.

Waziri  Mkuu Kassim Majaliwa  amekagua barabara ya kiwango cha lami  ya Inyonga   Mapili yenya  yenye  urefu wa zaidi ya kilometa 11 iliyogharimu shilingi bilioni  8.69 itayosaidia kuondoa changamoto kwa wajawazito  walikuwa nayo ya kuchewa kufika Hospitali pindi walipokuwa wameshindwa kujifungua na  kupelekea baadhi yao kupoteza  uhai.


Mwandisi Izack Kamwele mara baada ya kuelezea  manufaa ya barabara ya lami ya Inyonga Mapili mbele ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  amekagua barabara ya kiwango cha lami  ya Inyonga   Mapili yenya  yenye  urefu wa zaidi ya kilometa 11 iliyogharimu shilingi bilioni  8.69 itayosaidia kuondoa changamoto kwa wajawazito  walikuwa nayo ya kuchewa kufika Hospitali pindi walipokuwa wameshindwa kujifungua na  kupelekea baadhi yao kupoteza  uhai

Babarabara hiyo ni  sehemu ya barabara  Inyonga,Ilunde  Kishelo hadi Kitundaambako kuna  mapanda njia ya barabara  za kwenda Mbeya na Singida pamoja naTabora .  .

Akizungumza na wananchi wa Halmashauri ya Mlele mara baada ya kakagua Babara hiyo Waziri Mkuu Kassim alisema kuwa ameridhishwa na kiwango cha ubora wa ujenzi wa barabara hiyo .

Amebainisha kuwa lengo  la ujenzi wa barabara hiyo ni kuiunganisha  hadi  kwenye makutano ya barabara za  Mikoa ya  Tabora na Singida.

Na itawafanya wananchi wa Halmashauri ya Mlele kusafiri kwa kupitia njia hiyo kwenda Mkoani  pasipo kulazika kupitia Mpanda ambapo ni mbali zaidi .

Muonakano wa barabara aliyokagua Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya Inyonga Mapili

Amewakata wananchi waitunze vizuri barabara hiyo kwani ni mkombozi kwa wananchi

Mmoja wa wakazi wa  Kijiji cha Mapili  Domick Mbaruku  amemshukuru  Rais Dkt  Samia  Suluhu  Hassan kwa kuweza kutowa fedha za ujenzi wa barabara hiyo .

Kwani kukamika kwa barabara hiyo kutakuza uchumi wa wananchi na kwa Taifa  na kutaimarisha  huduma  za usafiri  wa  watu na mizigo.

Anna John anaishukuru  Serikali  kwa kuwajali husunani wananchi wa hali ya chini wakati wa masika mvua zikinyesha magari yalikuwa hayafiki na vifo vya wajawazito vilikuwa vingi   kwani walikuwa hawafiki  hospitali kwa wakati .

Walikuwa  wakipata wagonjwa usiku  walikuwa wanalazimika kuwabeba kwa machela wagonjwa wao .

Mbunge wa Jimbo la Katavi Mwandisi  Izack Kamwele alisema barabara hiyo ni muhimu sana kwa wananchi wa Mikoa ya Katavi,Tabora na Singida  na kwa Watanzania.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages