Kakulukulu
amesema wanaungana na Serikali katika kuhakikisha watoto wa Kitanzania wanapata
elimu na kwakuwa serikali imesha fanya kazi nzuri kwenye ujenzi wa miundo ya
madarasa katika kila eneo.
Ameeleza kuwa
wao kama viongozi wa dini katika mchango wa kuiunga mkono serikali wanaowajibu
wa kuhakikisha watoto wanaenda kusoma wakiwa kwenye mazingira mazuri ikiwa
nipamoja kupata vitendea kazi zikiwemo sale za shule.
Amesema “leo tupo hapa kwaajili ya kutoa sale za shule kwa watoto wa kike nawakiume kwa kuwapatia Shati na sketi na Kaptula kwakuzingatia kuwa hivi karibuni shule zinafunguliwa na tuwaone watoto hawa kama watoto wetu.”
Katika hatua nyingine ametoa wito kwa jamii na wadau mbalimbali kwa kuendelea kuwasaidia watoto wanaishi katika mazingira magumu katika suala la elimu kwakuwa elimu ni taa kwaajili ya maisha yao ya baadae.
Shekhe Mkuu wa Bakwata Mkoa wa Katavi Mashaka Nassoro Kakulukulu akikabidhi sale za shule kwa watoto wanaishi katika mazingira magumu wilaya ya Mpanda katika zoezi lililofanyika kwenye Viunga vya Msikiti mkuu wa Ijumaa Mpanda Katavi. [Picha na Goerge Mwigulu] |
Amewashukuru
viongozi wa Msikiti Mkuu wa Ijumaa Mpanda na wote waliochangia na hawana cha
kuwalipa mwenyezi Mungu atawalipa kwa kile walichotoa kwa watoto hao.
Hidaya
amebainisha kuwa kwa mara kadhaa amekuwa akiwalea watoto hao kwa yeye
kujishughulisha katika biashara ndogondogo kwa msaada huo umempunguzia kidogo
changamoto hiyo kwa watoto hao.
“Kabla ya
kupata huu msaada ninapambana mimi Bibi yao nahangaika biashara nakuhakisha
watoto wanakwenda shule kwa sasa namushukuru mwenyezi Mungu kila kitu kitaenda
sawa alisisitiza”
Asha kassimu
Mwanafunzi wa shule ya msingi nyerere nashukuru sana kwa msaada waliotupatia
mungu awabariki sana.