CCM KATAVI YATUMA SALAMU ZA PONGEZI KWA RAIS SAMIA

 

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa Katavi Idd Kimanta akiwahutubia wanachama wa chama hicho katika Kongamano la Kumpongeza Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa Kuondoa zuio la mikutano ya siasa Hapa nchini.

Na Paul mathias –Katavi

Chama cha Mapinduzi CCM katika mkoa wa Katavi kimempongeza Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia suluhu Hassani Kwa kitendo chake cha Kuondoa zuio la Kufanyika kwa mikutano ya kisiasa alilolitoa mnamo January 3,2023 Ikulu Jijini Dar es Salamu wakati akiongea na viongozi wa vyama vya siasa.

Baadhi ya wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa katavi wakiwa katika Kongamano la Kumpongeza Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutengua zuio la mikutano ya vyama vya siasa lililofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Mpanda Social hall wilaya ya Mpanda.

Akisoma Tamko hilo la pongezi kwa niaba ya wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM kwenye kongamano lililofanyika katika ukumbi wa Mapnada social hall Manispaa ya Mpanda Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Katavi amesema .

“Kwaniaba ya chama cha Mapinduzi mkoa wa Katavi na wanachama wa chama cha mapinduzi mkoa wa Katavi Tunampongeza na kumuunga Mkono Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kauli yake alioitoa Juzi 3,January 2023 ya kutengua zuio la kufanyika kwa Mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa, mkoa wa Katavi tunamuungamkono tupo pamoja nae katika kukuza Democrasia na kujenga umoja wa kitaifa”

Kimanta amesema  Rais Dkt samia Suluhu Hassan amekuwa mstari wa mbele kuionyesha Dunia kuwa watanzania tutaendelea kuwa wamoja na kuwa watulivu na kuendesha siasa zetu kwa amani ili nchizingine ziige mfano kutoka Tanzania

Ameeleza kuondolewa kwa hilo kusiwe chanzo cha vulugu na kuvunjiana heshima na kutukanana balikuewepo na siasa za kustahimiliana nakusisitiza  na chama cha mapinduzi kitanya mikutano yake kwa amani na utulivu

Ametoa wito kwa vyama vingine vya siasa kufanya mikutano yao kwa amani na utulivu kwa kuongozwa na hoja zenye kujenga na kuisadia serikali ya chama cha mapinduzi ili kutatua changamoto na kero zinazo wagusa wananchi moja kwa moja

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko wakati akisoma taarifa ya utekelezaji wa ilani ya chama chama cha Mapinduzi katika kongamano hilo amesema serikali imefanya mambo mengi ya maendelea katika sekta ya barabara kwa kuasaidia mkoa wa katavi kuunganishwa na mkoa wa Tabora kwa kiwango lami hali ianayopelekea kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mwanamvua Mrindoko akielezea utekelezaji wa ilani ya CCM katika mkoa wa Katavi kwenye Kongamano la Kumpongeza Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutengua zuio la mikutano ya hadahara.

Amebainisha  kukamilika kwa ujenzi wa bandari ya kalema kutaufanya mkoa wa katavi kuwa sehemu muhimu ya biashara baina ya nchi jiarani

Katika sekta ya Maji Mrindoko ameeleza kumekuwa na uboreshaji wa upatikanaji wa maji mijini na vijijini kwa kiwango kinachoridhisha kwa msukumo wa serikali ya wamu ya Sita ya Dkt Samia suluhu Hassan kuendelea kuleta Fedha kwaajili ya utekelezaji wa miundombinu hiyo

Awali akitoa neno  kwa niaba ya Wenyeviti wa halamsahauri kwenye kongamano hilo Mstahiki meya wa Manispaa ya Mpanda Haidary Summry amesema anatoa shukurani kwa Rais Dk samia suluhu Hassan kwa kuendelea kuleta fedha za miradi ya maendeleo katika halmashauri

Moja ya Bango lenye ujumbe kwa Rais Dkt Samia suluhu katika kongamano la kumpongeza kwa kutengua zuio la mikutano ya hadhara 

Sumry amesema kwa namna Maendeleo yanavyojionyesha kwa wananchi kumewapunguzia hoja za kwenda kujibu kwenye mikutano ya hadhara ambayo wapo tayari kwenda kuifanya na kusisitiza kuwa wapo tayari kujibu mapigo ya wapinzani kwa hoja katika majukwaa ya mikutano hiyo

Nae mbunge wa Viti maalumu mkoa wa katavi Martha Maliki amesema watakenda kuyasema yaleyote yananayofanywa na Serikali ya Dkt Samia suluhu Hassan kwa wanachi kwakuwa yanajipambanua kwa macho na kila mtu anayaona.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages