BILIONI 26.4 KUTATUA CHANGAMOTO ZA WANANCHI MPANDA.


Msitahiki meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Haidary Sumry akihutubia Kikao maalumu cha Kupitisha na Kupanga Rasimu ya Bajeti ya Halmashauri hiyo kwa Mwaka wa fedha wa 2023/2024[Picha na Paul Mathias]

Na Paul Mathias-Mpanda

Balaza la Madiwani katika halamsahauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi limepitisha kiasi cha shilingi Bilion 26.4 kwaajili ya kukusanya na kupokea kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2023/2024.

Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda wakiwa katika kikao maalumu cha kupitia na kupanga Rasimu ya Bajeti ya halamsahauri hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2023/2024 [PICHA na Paul Mathia]

Balaza la Madiwani katika halamsahauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi limepitisha kiasi cha shilingi Bilion 26.4 kwaajili ya kukusanya na kupokea kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2023/2024.

Akisoma Rasimu hiyo ya Bajeti kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Afisa Mipango wa halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Leonard Kilamuhama kwenye kikao maalumu cha cha Kupitisha na kupitia mpango huo wa Rasimu ya Bajeti amesema bajeti hiyo imejumuisha Makusanyo ya halmashauri kupitia mapato yake ya ndani fedha za serikali kuu na fedha mbalimbali kutoka kwa wafadhili. 

Kila muhama amesema katika Rasimu hiyo ya Mpango wa Bajeti Matumizi ya Kwaida Bilioni 17 huku Bilioni 9 zikitengwa kwaajili ya Miradi ya maendeleo katika Bajeti hiyo kupitia Mapato yake ya ndani halmashari ya Manispaa ya Mpanda imetenga Milioni 400 kwaajili ya Ujenzi wa Maboma 100 ya Mdarasa.

Afisa Mipango Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Leonard Kilamuhama akiwasilisha Rasimu ya Bajeti kwa Niaba ya Mkurugenzi Mtendaji kwenye kikao maalumu cha Balaza la Madiwani kuhusu bajeti ya halmashauri hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2023/2024[PICHA na Paul Mathias].
 
Pamoja na hayo halmashauri hiyo imetenga kiasi cha milioni 70 kwaajili ya Kuwalipa Wakandarasi mbalmbali madeni yao wanayoidai halmashauri hiyo halikadhalika kupitia mapato ya ndani zikitengwa Milioni 100 kwaajili ya kufungua Barabara kwenye Maeneo yaliyopimwa.

Msitahiki meya wa Manispaa ya Mpanda Haidary Sumry amesema Bajeti hiyo itakwenda kutekeleza Shughuli mbalimbali za Maendeleo ya wananchi wa Halmshauri ya Manispaa ya Mpanda na wao kama balaza la Madiwani wametimiza takwa hilo la kisheria la kupitisha rasimu hiyo ya bajeti.

“jumla kuu sasa inafanya jumla ya Bajeti ya jumla kwa maana ya Mapato ya ndani na mapato kutoka serikali kuu wafadhili na Mishara kuwa jumla ya shilingi bilioni 26.4 hivyo ndugu waandishi wa habari bajeti yetu imepita kama nilivyo eleza na itaendelea kwenye hatua zingine tukitoka kwenye baraza tunakwenda DCC na RCC kwaaajili ya kushauriwa”amesema Haidary

Diwani wa Kata ya Kawajense Uwezo Bachu akichangia hoja kwenye kikao maalumu cha kupanga na kupitisha Bajeti ya halmashauri ya Manispaa ya Mpanda [Picha na Paul Mathias]
Wiliamu Mbogo Diwani wa Kata ya Majengo halmshauri ya Manispaa ya Mpanda katika mchango wake kuhusu Bajeti hiyo ameiomba halmashauri kuendelea kutenga fedha katika eneo la kilimo cha Korosho kama zao la kimukakati ikiwa nisehemu ya kuwekeza kilimo hicho hasa kwa vijana.

Ukiangalia kwenye Bajeti hii naona imetengwa milioni 4 kwaajili ya hamasa kwa zao la Korosho fedha hii ahaitoshi kwa kilimo hiki kuweka hamasa kwenye zao la korosho

“kuna msemo wa kikonongo wengine wanakula wengine wanatimaza kwa macho hivyo tusije kuwa watazamaji wenzetu wa mikoa ya kusini wakiendelea kuvuana Mabilioni ya fedha kupitia kilimo hiki cha korosho”alihoji Mbogo.

Kwa upnde wake Uwezo Bachu Diwani wa kata ya Kawajense Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda amehoji mkataba wa Mradi wa kusindika nafaka katika eneo la kata ya Misunkumilo kutofanya kazi huku halmashauri ikiendelea kupoteza mapato.

Wiliamu Mbogo Diwani wa kata ya Majengo Manispaa ya Mpanda akichangia jambo katika Kikao maalumu cha kupanga na kupitisha Rasimu ya Bajeti ya Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda  [Picha na Paul Mathias]

Ameshauri Halmsahari kujipanga katika kuongeza Mashine za kukusanya Mapato POS pamoja na kuzingatia uwianao wa fedha zinazopelekwa kwenye kata kwa kuzingatia mahutaji yaliyopo.

Bachu ameishukuru serikali kwa kuendelea kutoa Elmu Bure kwa ngazi ya Shule ya Msingi Hadi Sekondari hali ambayo imewapa unafuu wanachi wenye watoto kuongeza hamasa ya kuwapeleka watoto wao shule.

Katibu tawala Mkoa wa Katavi Hassan Abas Rugwa akiwa Mgeni mwalikwa katika balaza hilo ameikumbusha halmashauri hiyo kuwa makini katika mikataba wanayo ingia hasa katika maeneo ya vibanda kwenda na wakati uliopo ili kuepuka kupoteza mapato ya halmashari.

Katibu Tawala Mkoa wa Katavi Hassan Abas Rugwa akitoa salamu za Mkoa wa Katavi alipoalikwa katika kikao maalumu cha kupitisha na kupanga Rasimu ya Bajeti ya halmashauri ya Manispaa ya Mpanda[Picha na Paul Mathias]
 
Rugwa ameshauri madiwani kwenda kusimamia usawa wa Mgawanyo wa fedha za halmashari kupitia mikopo ya vijana wanawake na wenye ulemavu kuzingatia miazania na kanuni zilizowekwa kwani “kunafedha zinaoneka lakini kulipwa kwake kumekuwa na changamoto hasa hizi zinatotolewa na halmashauri”.

 Mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila yusuph amelipongeza Baraza hilo kwa kupitisha bajeti hiyo huku akionya Taasisi za kifedha zinazo kopesha fedha kwa wananchi na kuanza kuawasumbua hato sita kuvifuta kwa kuwa baadhi zimekuwa zikinyanyasa wananchi pindi wanaposhidwa kulipa mikopo yao.

kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages